Na Ahmaid MMOW-Lindi 

Kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi oktoba mwaka huu,Mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel ten,Abdulaziz Ahmed leo Ametangaza nia yake ya kugombea ubunge katika jimbo la Lindi mjini katika uchaguzi mkuu ujao kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa,Abdulaziz ambae pia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Lindi alisema kuwa amefikia uamuzi huo baada ya kujitathimini na kugundua kuwa anao uwezo wa kuzikabili na kuzitafutia majibu yakinifu changamoto mbalimbali zilizopo katika jimbo la Lindi ambalo kwa sasa lipo chini ya Mbunge toka CUF,Salum Barwany.

"mwaka 2010 niliomba ridhaa ya kugombea ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi hata hivyo kura hazikutosha kupitia chama changu na Jimbo kuchukuliwa na Upinzani na nimeona changamoto nyingi zimeendelea kuwepo kwa miaka nenda rudi bila kutafutiwa ufumbuzi wa uhakika Nipeni Ridhaa wana lindi niwatumikie kuliko ilivyotokea katika matarajio yenu 2010-2015".

Aidha alibainisha changamoto hizo ni pamoja na miundombinu ya barabara,maji,huduma za afya na umeme usio na uhakika huku Akiainisha kuwa nguvu na uwezo wake kushinda katika kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi na uchaguzi mkuu zipo mikononi mwa wananchi wa jimbo hilo na ambao wanakiu ya maendeleo na mabadiliko.

" sitegemei kutumia Fedha ili kuwa nunua wapiga kura bali wale wapenda maendeleo na mabadiliko ndiyo mtaji na silaha yangu,rushwa hapana kwani chama chetu hakitaki kabisa kitendo hicho kwa kuwa kinaathiri Maendeleo na kinaua chama cha Mapinduzi kwa Uwepo wa Makundi yanayotaka kupona maisha yao tu si maendeleo.

Aidha alitoa wito kwa Vijana kujitokeza kwa wingi kujiandikisha huku wengine wakijiunga na Chama hicho ili kumpigia kura Mgombea ambae anatoka katika kundi la Vijana kwa kuwa Vijana ndio Taifa la leo.

Sambamba na hilo Abdulaziz aliziasa kamati za chama na vikao vya uteuzi kuzingatia matakwa na maamuzi ya wanachama huku akikemea matumizi ya fedha kwa wagombea kuhonga wanachama ili wawapigie Kura. 

"Mpango huu wa kuhonga wanachama una athari kubwa kwa Chama Pia upo uwezekano wa kupata mgombea asiekubalika na kuendelea kutwaliwa na Upinzani ni lazima tuwe makini katika hili,Nina Imani hata Vijana toka vyama vya Upinzani wataniunga mkono na kunichagua kuwawakilisha".Alimalizia Abdulaziz alipokutana na waandishi wa habari wa Vyombo Mbali mbali

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...