Muimbaji wa Nyimbo za Injili Rehema Chawe

MSANII wa nyimbo za Injili, nyanda za juu kusini Rehema Chawe ambaye ni Mwanachama wa chama cha Muziki wa Injili Tanzania (CHAMUITA), anatarajia kuzindua albamu yake ya kwanza, inayoitwa Kusamehe ni afya.


Uzinduzi huo unatarajia kufanyika Jumapili, March 8, mwaka katika kanisa la EAGT, Frelimo kwa mchungaji Mwenda, ambaye ni Mwenyekiti wa makanisa ya Kipentekoste mkoani Iringa.


Akizungumza na wanahabari, Chawe alisema uzinduzi huo utapambwa na waimbaji wengi toka nje na ndani ya mkoa wa Iringa.


Alisema mgeni rasmi katika uzinduzi huo atakuwa, ni mhadhiri wa chuo kikuu cha Iringa, Enock Ugulumo.


Mwenyekiti wa CHAMUITA mikoa ya nyanda za juu kusini, Tumaini Msowoya Kibiki aliwataka wanachama wote kuwepo kwenye uzinduzi huo ili kumsindikiza mwenzao.


“Ni jukumu la waimbaji wote hususani wanachamuita kuhakikisha wanakuwepo siku ya uzinduzi ili kumuunga mkono mwanachama wenzetu,”alisema Kibiki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...