Akizungumza na DjHaazu wa Mambo Jambo Radio Arusha Kupitia Kipindi cha DUNDO Choka amesema NITALALA UZEENI ni wimbo flani unaoelezea Zaidi jinsi ambavyo Watu wanaHustle kila kukicha na Kula Bata huku wakiamini Hakuna kulala Kwani Kulala kuko Uzeeni.
Ngoma hiyo imefanywa pale AM Records na amewapa Shavu Vijana Wapya kwenye Game ambao ni Young Mlunya na Big Y Na wawili wengine ambao wanajulikana ni Country Boy na Climax Bibo.
Hata hivyo Choka amezungumzia pia Ukimya aliokuwa nao kwenye Utoaji wa Zile Project zake kuwa ni Majukumu na kukaa Karibu na Familia huku akihakikisha kuwa anakaa karibu zaidi na Mwanaye ili asije akaitwa Uncle na Mwanae kwa kukaa Mbali naye.
Kitamu zaidi ni kwamba Kuna Mbali na hiyo Pia Kuna Project Zingine Zinazofuata Soon Kupitia Mikono ya Maproducer tofauti ambao Tayari ameshakaa nao Sawa ambao ni Mesen Selekta, NahReal na Kwakuwa hana Mpango wa Kufanya Kubum Kubaa sana ila lazima afanye Mkono Mmoja wa KubumKuban kutoka Kwa Producer Mkali wa Hip-Hop Toka Arusha DAZ NALEDGE Toka DabMusic
PATA NAFASI YA KUMSIKILIZA DJ CHOKA AKIZUNGUMZA NA DJHAAZU KWA KU-CLICK LINK HII>>> DJ CHOKA NDANI YA MAMBOJAMBO RADIO NA @DJHAAZU
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...