Mkurugenzi Mtendaji wa Muda wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Pius Tibazarwa (katikati) akikabidhi funguo kwa mshindi wa zawadi kubwa ya promosheni ya Weka Upewe, Josephat Ruyongo mkazi wa Bukoba, ya gari lake jipya alilojishindia la Nissan Hardbody katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa NBC, Mussa Jallow. Gari hilo lina thamani ya zaidi ya sh milioni 54.
Mshindi wa zawadi kubwa ya promosheni ya Weka Upewe ya Benki ya NBC, mkazi wa Bukoba, Josephat Ruyongo akifungua gari lake mara baada ya kukabidhiwa rasmi na Mkurugenzi Mtendaji wa Muda wa NBC, Pius Tibazarwa (katikati), jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa NBC, Mussa Jallow.
Mshindi wa zawadi kubwa ya promosheni ya Weka Upewe ya Benki ya NBC, mkazi wa Bukoba, Josephat Ruyongo akiwasha gari lake tayari kwa safari ya Bukoba mara baada ya kukabidhiwa jijini humo leo.
Mshindi wa zawadi kubwa ya promosheni ya Weka Upewe ya Benki ya NBC, mkazi wa Bukoba, Josephat Ruyongo (katikati) akipozi kwa picha ya kumbukumbu pamoja na baadhi ya maofisa wa benki hiyo mara baada ya kukabidhiwa gari lake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Hongera mshindi kwa kukabidhiwa zawadi ya gari. Promosheni hizi ni nzuri.

    ReplyDelete
  2. jamani itabidi afundishwe kuendesha kabla hajapewa gari. maana ajali kibao siku hizi.

    ni hayo tuuuu.

    asante

    Msemakweli

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...