Gari ya Serikali aina ya Toyota Land Cruser yenye namba za Usajili STK 7278, ikiwa imeparamia ukuta wa Shule ya msingi Al Muntazir iliyopo kwenye makutano ya barabara ya Sea View na Barack Obama Drive, jijini Dar es salaam. Kwa mujibu wa mashuhuda dereva wake alijikuta hana jinsi ila kutoka barabarani kuepusha mzinga swa uso kwa uso wakati alipochomekewa ghafla na gari nyingine ya teksi ambayo baada ya kusababisha ajali hii iliingia mitini. Ajali hii imetokea jioni ya leo wakati gari hili likiwa linatokea mjini kuelekea upande wa Palm Beach. Hakuna aliejeruhiwa katika ajali hii.
Wafanyakazi wa "Break Down" wakiangalia namna ya kuichomoa gari hiyo iliyoparamia ukuta wa Shule ya msingi Al Muntazir iliyopo kwenye makutano ya barabara ya Sea View na Barack Obama Drive, jijini Dar es salaam leo.
Hivi ndivyo ionekanavyo gari hiyo mara baada ya kuchomolewa kwenye ukuta huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...