Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Rais-Ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Miradi (PDB) inayosimamia utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN),  Omari Issa amewashauri Wakuu wa Nchi za Ukanda wa Kati wa Uchukuzi kuwa mifumo ya ufuatiliaji na utekelezaji itakayoharakisha ukamilishaji wa miradi iliyoko katika nchi zao.

Alisisitiza kuwa bila kuwa na mifumo ya ufuatiliaji, baadhi ya nchi zinaweza kumaliza kwa wakati miradi yake; huku nchi nyingine zikichelewa kukamilisha miradi iliyo upande wake. Hali hii inaweza kuzivunja moyo nchi ambazo zitakuwa zimekamilisha miradi yake, hasa ikizingatiwa kwamba miradi yote ya Uchukuzi ya Nchi za Ukanda wa Kati inategemeana.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana wakati wa Majadiliano ya Wakuu wa Nchi za Mpango wa Uharakishaji wa Ujenzi wa Miundombinu katika Ukanda wa Kati, Bw. Issa alisema Tanzania imetekeleza miradi mbalimbali katika mwaka wa kwanza wa BRN kuliko ilivyotarajiwa kwa kutumia bajeti kidogo kutokana na nidhamu ya utekelezaji chini ya mfumo huo wa BRN, unaosisitizia katika kuweka vipaumbele, ufuatiliaji madhubuti na utatuzi wa changamoto. Nidhamu hiyo imesaidia kutatua changamoto zilizokuwa na zinazooendelea kujitokeza; na kuifanya Tanzania iweze kutekeleza kwa ufanisi miradi yake ya kipaumbele ikiwemo ile iliyo katika sekta ya uchukuzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. We are such a great country. Hivi haya BRN wanayoyafanya Wizara ya Mipango ama Hazina wameshindwa kuyafanya?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...