SHIRIKA LA MAJI SAFI NA MAJITAKA DAR-ES-SALAAM (DAWASCO),
LINAWATANGAZIA  WAKAZI WA JIJI LA DAR-ES-SALAAM NA MJI WA BAGAMOYO MKOANI PWANI  KUWA, MTAMBO WA KUZALISHA MAJI WA RUVU CHINI UMEZIMWA KWA SAA 24 KUANZIA ASUBUHI YA TAREHE 01.03.2015. 

KUZIMWA KWA MTAMBO WA RUVU CHINI KUMETOKANA NA MATENGENEZO YA BOMBA LA INCH 54 ENEO LA MATANKI YA CHUO KIKUU.

MATENGENEZO YANAENDELEA NA YANATARAJIA KUKAMILIKA BAADA YA SAA 24.

 KWASABABU HIYO MAENEO YAFUATAYO YATAKOSA MAJI:
MJI WA BAGAMOYO, VIJIJI VYA MAPINGA, KEREGE NA MAPUNGA. BUNJU, BOKO, TEGETA, KUNDUCHI, SALASALA, JANGWANI, MBEZI BEACH NA KAWE.
MAENEO MENGINE NI MLALAKUWA, MWENGE, MIKOCHENI, MSASANI, SINZA, MANZESE, MABIBO, KIJITONYAMA, KINONDONI, OYSTERBAY, MAGOMENI, UPANGA, KARIAKOO, CITY CENTRE, ILALA, UBUNGO MAZIWA, KIGOGO, MBURAHATI, HOSPITALI YA RUFAA MUHIMBILI, BUGURUNI, CHANGOMBE NA KEKO.       
         
WANANCHI MNASHAURIWA KUHIFADHI MAJI NA KUYATUMIA KWA MATUMIZI YA LAZIMA.

DAWASCO INAWAOMBA RADHI KWA USUMBUFU UTAKAOJITOKEZA
KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA SIMU HUDUMA KWA WATEJA 022 5500240-4 NA 0658-198889

IMETOLEWA NA OFISI YA UHUSIANO
DAWASCO-MAKAO MAKUU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. This is the reason a third world country will remain so,then what do u do after the water is shut off,meaning you cant flash your toilet,cant shower,its a life distraction,when will these DAWASCO Figure out to attend on an emergency like this? When will they built reserve dams?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...