Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF unaendelea kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari ili waweze  kutumia vyombo vya habari vilivyoko kwenye maeneo yao kutangaza habari za Mpango wa kunusuru kaya masikini unaoratibiwa naMfuko huo.

Akifungua mafunzo hayo yanayoendeshwa kwa utaratibu wa Kikao Kazi Mkurugenzi Mtendajiwa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga amesema kazi ya kutokomeza umaskini nchini inahitaji ushiriki wa wadau mbalimbali vikiwemo vyombo vya habari.

Bwana Mwamanga amesema tangu TASAF ianze kutekeleza Mpango wa kunusuru kaya masikini kumekuwa na mafanikio makubwa hususani katika maeneo ya walengwa ambao wameanza kuboresha maisha yao na katika baadhi ya maeneo walengwa wameanza kukuza shughuli za kiuchumi huku wengine wakiweza kuhudumia kaya zaokinyume na hali ilivyokuwa huko nyuma.

Amewasihi waandishi wa habari kuwatembelea walengwa wa Mpango huo ili kuona namna walengwa hao wanavyonufaika na Mpango huo wa uhawilishaji fedha na kisha kutangaza mafanikio yaliyokwisha patikana huku akisisitiza kuwa hata pale penye changamoto zionyeshwe ili marekebisho yafanyike kwa manufaa ya walengwa
Zifuatazo ni baadhi ya picha za washiriki wa kikao kazi hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Chuo kikuu Huria Mjini Mtwara.
 Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bwana RenatusMongogwela (mwenye shati nyeupe)akizungumza na ujumbe wa TASAF ulioongozwa na Mkurugenzi mtendaji Ladislaus Mwamangawa, kwanza kushoto kwa kaimu katibu tawala.
  Mkurugenzi Mtendajiwa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga aliyesimama akifungua kikao kazi cha watendajiwa TASAF kutoka maeneo ya utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya maskini na waandishi wa habari wa mikoa ya Mtwara na Lindi (hawapopichani) 
 Washiriki wa kikao kazi cha watendaji wa TASAF  na waandishi wa habari kutoka mikoa ya Mtwara na Lindi wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga(hayupo pichani).
 Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF bwana  Ladislaus Mwamanga akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa TASAF makao makuu baada ya kufungua kikao kazi cha waandishi wa habari wa mikoa ya Mtwara na Lindi.
 Mkurugenzi Mtendajiwa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa TASAF makao makuu baada ya kufungua kikao kazi cha waandishi wa habari wa mikoa ya Mtwara na Lindi.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...