WAZIRI wa Ujenzi Dkt. John Magufuli ametoa siku 14, kwa Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), kuanza ukarabati wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Siha na Moshi baada ya kubainika majengo hayo kujengwa chini ya kiwango.

Dkt. Magufuli pia ameagiza aliyekuwa meneja wa TBA Mkoa wa Kilimanjaro, Paul Ndossa kusimamishwa kazi mahali alipo ili arejee kujibu tuhuma na kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria.

Waziri huyo alitoa agizo hilo wakati akikagua jengo la mkuu wa Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro baada ya kupewa taarifa za jengo hilo kujengwa chini ya kiwango hali iliyosababisha shughuli za mkuu wa Wilaya ya Siha kuhamishiwa kwenye ofisi za maji za halamashauri hiyo.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji mkuu wa TBA Elius Mwakalinga alisema wakala hao wanasikitishwa na kasoro za kiufundi zilizojitokeza katika jengo hilo na watawachukulia hatua wote waliohusika katika kuchangia majengo hayo kuwa chini ya kiwango.

Mwakalinga amesema tayari TBA imefanya tathmini ya gharama za ukarabati wa jengo la Wilaya ya Siha ambao utafanyika katika kipindi cha wiki 18 na kugharimu shilingi milioni 50.

Majengo ya ofisi za wakuu wa Wilaya za Siha na Moshi yalijengwa kwa usimamizi wa TBA ambapo wahusika walishindwa kuyatumia wakihofia usalama wao baada ya kuona dosari.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hongera sana Mh Dkt Mangufuli kwa utendaji wako wa kazi. Chakushangaza nikwamba mpaka majengo haya yanakamilika na kukabidhiwa katika kiwango cha chini, Eng wa wilaya,Mh DC, Katibu Tawala,Waheshimiwa madiwani walikuwa wapi?? Ingependeza sana kama na wenyewe wangewajibishwa. Mali za serikali nilazima tuwe na uchungu nazo,nikodi za walala hoi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...