Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Eng. Patrick Mfugale amesema hakuna ufisadi wowote wala malipo tata yaliyofanywa na wizara ya ujenzi kwa makandarasi na wahandisi washauri katika bajeti ya mwaka 2011/2012.

Eng. Mfugale amesema fedha zote zilizotengwa kwa ajili ya kasma maalum ya ujenzi wa miradi ya barabara nchini kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 252 kilitumika kulipa madai ya Makandarasi na Wahandisi washauri.

Eng. Mfugale amesisitiza kuwa Serikali inajenga barabara kwa kuzingatia vipaumbele vya maendeleeo na hulipa makandarasi na wahandisi washauri ili kuwezesha kazi hizo kufanyika kwa wakati na kwa kuzingatia mikataba.

Eng. Mfugale ametoa ufafanuzi huo kufuatia baadhi ya vyombo vya habari kunukuliwa kuwa kumekuwa na ubadhirifu ,au matumizi tata katika malipo ya wakandarasi Wizara ya Ujenzi na kusisitiza kuwa suala hilo lilishajadiliwa na kupatiwa ufumbuzi na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), katika kikao chake cha Agosti 22 mwaka 2013.

Amewataka watumishi wa TANROADS kote nchini kuendelea na shughuli zao za ujenzi na usimamizi wa barabara bila kuvunjika moyo kwani hakuna ubadhirifu wowote.

Zaidi ya km 35,000 za barabara hapa nchini zinasimamiwa na TANROADS kupitia mameneja wake katika mikao 25 nchini kote ambapo takriban KM 11,154 zinajengwa kwa kiwango cha lami katika kipindi hiki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Jamani fukieni mashimo kupunguza ajali kama iliyotokea Mafinga leo...hii ajali sio uzembe wa madereva..haya mshimo yamekuwa kwa muda mrefu. Viongozi wanapita...mabosi wakubwa tu wanapita jamani hii ni barabara kuu inayotegemewa sana hapa nchini mwetu...Tafadhali zingatieni hili..na kulifanyia kazi..kama yale mashimo yangezibwa hii ajali ingeweza kuepukika

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...