Mwenyekiti wa Unity Women Foundation (UWF), Maryam Ajmy akiwa akikusanya misaada waliyokuwa wakitoa katika hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam kutoa msaada kwa wanawake ikiwa ni kuadhimisha siku ya wanawake duniani iliyofanyika hivi karibuni.  
Mwenyekiti wa Unity Women Foundation (UWF), Maryam Ajmy akiwa na wanaumoja wenzake wakiingia hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam kutoa msaada kwa wanawake ikiwa ni kuadhimisha siku ya wanawake duniani iliyofanyika hivi karibuni.   
---
Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Unity Women Foundation (UWF), umetoa msaada kwa wanawake wagonjwa katika hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na baada ya kutoa msaada katika Siku ya Wanawake Duniani iliyofanyika hivi karibuni, Mwenyekiti wa UWF, Mariam Shamo amesema wanawake wanatakiwa kujitoa kwa wanawake wenzao wenye matatizo kwa siku zote kutokana na kuwepo kwa wanawake wengine hawana msaada wa mtu yeyote.

Mariam amesema wanawake siku ya wanawake itumike kwa kwa kufariajiana na kuendelea na kuweza kuona kuona mabadiliko na kuweza kutatua changamoto zetu zinazotukabiri.Amesema wanawake wenye uwezo wasaidie na kuwatembelea wanawake wenzao katika wodi mbalimbali na kutoa msaada hata kama ni kidogo lakini kinathamani yake.
Aidha amesema kama UWF wataendelea kutoa kuwafariji wagonjwa kila muda ili nao waweze kujua wanawake wa nje yao wanatambua matatizo yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kasoro maji (kidogo), lakini hivyo vitu vingine havifai kabisa kwa wagonjwa, hasahasa wa aina ya wagonjwa wa kansa! Kabla ya kutoa msaada ni vyema kulijua hilo!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...