Umati wa Washabiki wa Timu ya Simba ukiwa umefurika uwanja wa Taifa jijin Dar es salaam kuipa sapoti timu yao ambayo haikuwaangusha leo,baada ya kuwatandika bao 1 - 0 watani zao wa jadi Yanga,lililotiwa kimiani  kwa umaridadi mkubwa na Mshambuliaji,Emmanuel Okwi mnamo dakika ya 52 ya mchezo.
 Beki wa Timu ya Simba,Kessy Ramadhan akiwania mpira na Mshambuliaji wa timu ya Yanga,Danny Mrwanda wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.Simba imeshinda bao 1 - 0 lililotiwa kimiani  kwa umaridadi mkubwa na Mshambuliaji,Emmanuel Okwi mnamo dakika ya 52 ya mchezo.PICHA NA OTHMAN MICHUZI.
 Mshambuliaji wa timu ya Yanga,Danny Mrwanda akijaribu kumtoka Beki wa Timu ya Simba,Kessy Ramadhan wakati wa mchezo wa Ligi kuu Tanzania Bara uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
 Nyanda nambari moja wa timu ya Simba,Ivo Mapunda akiwa ametulia langoni kwake tayari kwa kuzuia shuti lililopigwa na Mshambuliaji wa Yanga,Simon Msuva.

KUONA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...