Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa amri kuzindua rasmi meli vita mbili za doria bahari kuu TNS Msoga na TNS Mwitongo kwenye sherehe zilizofanyika Kamandi ya Jeshi la Maji Kigamboni jijini Dar es salaam leo April 28, 2015
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua mara baada ya kuzindua rasmi meli vita mbili za doria bahari kuu TNS Msoga na TNS Mwitongo kwenye sherehe zilizofanyika Kamandi ya Jeshi la Maji Kigamboni jijini Dar es salaam leo April 28, 2015
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata picha ya kumbukumbu na makamanda wa meli vita mbili za doria bahari kuu TNS Msoga na TNS Mwitongo kwenye sherehe zilizofanyika Kamandi ya Jeshi la Maji Kigamboni jijini Dar es salaam leo April 28, 2015
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Chifu Edward Wanzagi wa kabila la Wazanaki (kati) pamoja na Mbunge wa Afrika Mashariki Mhe Makongoro Nyerere baada ya kuzindua rasmi meli vita mbili za doria bahari kuu TNS Msoga na TNS Mwitongo kwenye sherehe zilizofanyika Kamandi ya Jeshi la Maji Kigamboni jijini Dar es salaam leo April 28, 2015. PICHA NA IKULU
---------------------------------
---------------------------------
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Jumanne,
Aprili 28, 2015, ametoa kamisheni na kuruhusu kuanza kutumika kwa Melitiva
mbili kwa ajili ya ulinzi wa pwani ya Tanzania.
Rais Kikwete
ametoa kamisheni hiyo na kuruhusu kuanza kutumika kwa meli hizo, Melivita P77
Tanzania Navy Ship Mwitongo na Melivita P78 Tanzania Navy Ship Msoga katika
Sherehe ya Utoaji Kamisheni iliyofanyika Makao Makuu ya Kamandi ya Jeshi la
Maji la Tanzania Navy Base, Kigamboni, mjini Dar es Salaam.
Mkuu wa
Majeshi ya Ulinzi (CDF) Jenerali Davis Mwamunyange na Balozi wa China katika
Tanzania, Balozi Lu Youching walikuwa miongoni mwa waliohudhuria sherehe hizo
pamoja na wawakilishi wa kijiji cha Mwitongo, Butiama Mkoani Mara na Kijiji cha
Msoga, Wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani ambavyo majina yake yametolewa kwa meli
hizo mbili.
Akizungumza
katika sherehe hizo, Jenerali Mwamunyange amesema uongozi wa Jeshi umeamua
kuziita meli hizo mbili kubwa zaidi za kivita zilizopata kununuliwa nchini
majina ya vijiji walikozaliwa viongozi wakuu wawili wa Tanzania, Mwalimu Nyerere
na Rais Kikwete.
Rais Kikwete
ameambiwa katika shehere hizo kuwa meli hizo kutoka Jamhuri ya Watu wa China,
zitaongeza kwa kiwango kikubwa uwezo wa JWTZ kulinda mpaka wake ulioko katika
Bahari ya Hindi na kuweza kukabiliana zaidi na vitendo vya uharifu, ugaidi
na kulinda vizuri zaidi shughuli za
utafutaji gesi na mafuta katika pwani hiyo ya Tanzania.
Akizungumza
kabla ya kutoa kamisheni kwa meli hizo, Rais Kikwete ameishukuru Jamhuri ya
Watu wa China kwa kuendelea kuiunga mkono Tanzania katika Nyanja ya kijeshi na
Nyanja nyingine nyingi.
“Marafiki zetu
wa China wamekuwa nasi kwa muda mrefu, wametuunga mkono tokea kuanzishwa kwa
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania tokea Mwaka 1964. Kwa upande wa ulinzi
wa majini, wamekuwepo tokea Mwaka 1971 walipotusaidia kuanzishwa kituo hiki cha
Tanzania Naval Base hapa Kigamboni na kutoa boti 13 za ulinzi.”
Ameongeza Rais
Kikwete: “Wamesaidia vifaa, wamesaidia utaalam na wataalam, wametoa mafunzo
katika Chuo chetu cha Ubaharia cha hapa hapa. Kwa hakika hakuna marafiki kama
wenzetu wa China, wananchi wake na Serikali yake kwa sababu wamesaidia sana
maendeleo ya Jeshi letu. Karibuni wametusaidia kuanzisha kombania mbili za
majeshi maalum ya majini na sasa meli hizi mbili ambazo zina uwezo wa kwenda
kasi zaidi, uwezo wa kubeba silaha nyingi na kubwa zaidi na uwezo zaidi wa
kulinda mipaka yetu”.
“Wako watu
wanasema kuwa vifaa vya jeshi na ulinzi wa nchi yetu ni ghali. Ni kweli. Lakini
sasa nani atatulindia nchi yetu? Ni sisi wenyewe na kazi ya ulinzi wa nchi
haiweza kuwa kazi rahisi, wala nyepesi, wala isiyokuwa na gharama.”
Akifafanua
hali ilivyo katika Pwani ya Tanzania, Rais Kikwete amesema: ”Miaka
ya karibuni hapa yaliwahi kutokea majaribio 28 ya kuteka nyara meli katika eneo
la maji la Tanzania, matano yalifanikiwa na mengine yakashindikana. Tuna
shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi, maharamia hufanya jitihada za kuzivuruga, lazima
tuzilinde.”
Akitoa
kamisheni hiyo, Rais Kikwete amesema: “Kwa
kutumia nafasi yangu kama Amiri Jeshi Mkuu, natoa kamisheni na kuruhusu kuanza
kutumika kwa melivita P77 Mwitongo na P78 Msoga. Mwenyezi Mungu azibariki
melivita hizi pamoja na wafanyakazi wake wote.”
Wakati wa
ukaguzi wa meli hizo, Rais Kikwete ameambiwa kuwa kila moja ya meli hizo ina
uwezo wa kukaa baharini kwa muda wa siku saba bila kuhitaji kuongeza mafuta
wala diseli na bila kuhitaji msaada wa huduma yoyote kwa ajili ya watumishi
wake.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu
– Dar es Salaam.
28 Aprili,2015
Maafa ya majini yakitokeaga..huwa tu wapweke kama hatuna navy.........
ReplyDeleteavenue na ndege .za kisasa kila la kheri .TZ
ReplyDeleteIPO siku tutazpga mkwara nchi jiran kama kenya heshma silaha tu