Balozi wa Tanzania Ubeligiji, Laxembourg na Jumuiya ya Ulaya Dr.
Diodorus Buberwa Kamala (wa kwanza kushoto) akiwa katika picha ya pamoja
na Viongozi Kutoka Nchi Mbamlimbali Duniani Baada ya Ufunguzi Rasmi wa
Kongamano la Biashara la Kimataifa linalofanyika Genval Ubeligiji.
Makampuni zaidi ya 500 yakiwemo hamsini kutoka Tanzania yanashiriki
Kongamano hilo.
Makampuni hapo yanatoka nchi zinazozungumza kifaransa.
Tanzania ni nchi pekee inayozungumza kingereza iliyokaribishwa
kushiriki. Kesho, Balozi Kamala atawasilisha mada ya kubainisha fursa za
uwekezaji na biashara zinazopatikana Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...