Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na
Watoto,Mhe.Dkt.Pindi Chana akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa
Kompyuta katika Chuo cha Maendeleo ya
Wananchi Arnautoglu kilichopo Manispaa
ya Ilala,leo jijini Dar es Salaam.
Meneja Masoko na Maendeleo ya Bidhaa wa DCB
Commercial Bank,Bw.Boyd Mwaisame akifafanua jambo wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa
Kompyuta katika Chuo cha Maendeleo ya
Wananchi Arnautoglu kilichopo Manispaa
ya Ilala,leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Arnautoglu
wakisikiliza kwa makini risala iliyo kuwa ikisomwa na Naibu Waziri wa Maendeleo
ya Jamii Jinsia na Watoto,Mhe.Dkt.Pindi Chana leo Jijini Dar es Salaam.
0
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na
Watoto,Mhe.Dkt.Pindi Chana (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na uongozi
wa Chuo Cha Maendeleo ya Wananchi Arnautoglu
kilichopo Manispaa ya Ilala,leo jijini Dar es Salaam.( Picha na Emmanuel
Massaka)
Na Bakari Issa,Dar es Salaam.
Benki ya Biashara ya DCB imetoa msaada wa Kompyuta kwa Chuo
cha Maendeleo ya Wananchi Arnautoglu
kilichopo Manispaa ya Ilala,kwa lengo la kutoa elimu katika Chuo hiko
chenye wanafunzi wenye ulemavu.
Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo wa
Kompyuta kwa Chuo hicho,Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto,Mhe.Dkt.Pindi
Chana amesema umuhimu wa Vyuo hivi
unatokana na lengo la kuanzishwa kwake aambalo ni kutoa maarifa na stadi
zitakazowawezesha wananchi kujiajiri,kujitegemea ili kuondokana na ujinga,umaskini na maradhi
hatimaye waweze kuchangia kuinua uchumi wa taifa.
Pia,Dkt.Chana amewahasa wazazi kuacha kuwaacha watoto wao
kukaa nyumbani bila kujishughulisha na shughuli yeyote pindi wanapomaliza
masomo yao na badala yake kuwashughulisha watoto hao ili kujiepuka kujiingiza
kwenye makundi yasiyofaa.
Kwa upande wake,Meneja Masoko na Maendeleo ya Bidhaa wa DCB
Commercial Bank,Bw.Boyd Mwaisame amesema
Benki imekabidhi msaada huo kutokana na kuguswa na matatizo mengi
yanayojitokeza katika jamii likiwemo la ukosefu wa vitendea kazi . kwa watoto
wenye Ulemavu.
Naye, Mkuu wa Chuo
hiko,Bi.Pulcheria M. Ndamgoba ametoa
shukrani kwa msaada huo wa Kompyuta katika Chuo hiko na kuahidi
kukitumia vizuri katika kutoa elimu chuoni hapo,huko Kiongozi wa Wanafunzi wa Chuo hiko,Ridhwan Omary akitoa
msisitizo kwa Benki hiyo kuwasaidia kujengea viwanja vya michezo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...