Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

MKURUGENZI Mtendaji wa Kampuni ya Reli nchini(TRL),Mhandisi Kapallo Kisamfu amesimamishwa kazi kupisha uchunguzi wa malipo ya Sh. Bilioni 230 ya mabehewa ya Mizigo yenye kasoro pamoja na kufanya malipo ya mabehewa yote kabla ya kukamilika.

Akitangaza maamuzi hayo ya kusimimishwa kwa Mkurugenzi huyo leo jijini Dar es Salaam baada ya ripoti ya kamati iliyoundwa na Waziri wa Uchukuzi (ambaye sasa ni Waziri wa Afrika Mashariki), Dk. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Uchukuzi,Samwel Sitta amesema ameshtushwa na malipo hayo kwani yamekiuka manunuzi ya umma kwani mkataba wake ulikuwa TRL ilipe nusu ya asilimia 50 lakini matokeo yake mabehewa yamelipwa yote.

Amesema mabehewa 120 yaliyofika nchini yakiwa yana kasoro aliyazuia baada ya kubaini hivyo lakini TRL ilikuwa imeshalipa fedha yote katika mazingira hayo yanaonyesha mkataba una dalili ya hujuma.

Waliosimamishwa wengine ni Mhandisi Mkuu wa Mitambo TRL,Ngosomwile Ngosomiles,Mhasibu Mkuu,Mbaraka Mchopa ,Mkaguzi Mkuu wa Ndani Jasper Kisiraga pamoja na Meneja Mkuu Ferdinand Soka.

Kamati ya uchunguzi kwa watendaji hao kwa kuidhinishwa kwa kulipwa kwa mabilioni ya Shilingi itaongozwa na Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),Taasisi ya Kupambana na Rushwa (Takukuru),Mamlaka ya udhibiti wa Ununuzi katika sekta ya Umma (PPRA),pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Waziri wa Uchukuzi,Samwel Sitta akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana kuwasimamisha baadhi ya watendaji wakuu wa kampuni ya Reli hapa nchini uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Uchukuzi,Samwel Sitta akionyesha baadhi ya Ripoti za uchunguzi za mamlaka ya Bandari,TPA na Ripoti ya shirika la Reli jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya Waandishi wa Habari walio hudhuria katika mkutano wa Waziri wa Uchukuzi,Samwel Sitta katika wizara hiyo jijini Dar es Salaam leo.(Picha na Avila kakingo)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...