Na. Wambara Mayori, Pwani.
   
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Bi Subira Khamis Mgalu, amewasihi wananchi wa  Kisarawe kulinda ardhi yao kama mboni ya jicho  na kuwataka kuacha tabia ya kuuza ardhi yao kiholela na badala yake wajikite katika kuyaendeleza maeneo yao. 

Bi Subira, amesema kuwa, kuna watu hutumia kofia ya uwekezaji katika nchi hii kujitwalia ardhi katika maeneo mbalimbali  na kisha kuyatelekeza bila ya kufanyiwa kazi kwa muda mrefu na kuleta usumbufu mkubwa kwa wananchi wanaoishi kuzunguka maeneo hayo kwa kugeuka kuwa  mazalia na makazi ya nyoka , maficho ya wahalifu na baadaye kuwa chanzo cha migogoro ya ardhi alisema.

Alisema, hatuhitaji wawekezaji wasio na tija kwa wananchi wa wilaya ya Kisarawe, na kusisitiza kuwa muda wa wawekezaji hewa umekwisha na wala hatuhitaji wawekezaji wanaokuja na mikoba bali tunawakaribisha wawekezaji wenye tija wanaoweza kutoa fursa ya ajira kwa wananchi na vijana wa wilaya ya Kisarawe.

Hata hivyo, ametoa wito kwa wenyeji na wakazi wa wilaya hiyo kutokuwa wepesi kununulika kwa watu wajanja wachache wanaojiita wawekezaji na badala yake wawe macho na watu hao ili wasijikute wanapoteza ardhi yao.

Aidha, Mkuu huyo wa wilaya, amewaonya viongozi wanaokumbatia wawekezaji hewa katika wilaya hiyo na   amewataka wananchi kushikamana na  kushirikiana na viongozi wao wa vijiji na mitaa katika kupanga na kusimamia  mipango yao ya maendeleo kwenye maeneo yao kwani maendeleo yao ni maendeleo ya wilaya ya Kisarawe, alisema.

Alisema, Bi Subira, ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Homboza        kilichopo Kata ya Msimbu Tarafa ya Sungwi wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, huku akiwatahadhalisha kuwa, hakuna mtu yeyote anayeweza kumkataza ama kumnyima mtu haki yake ya kikatiba ya kuchagua kiongozi anayemtaka kwa kuwa hiyo ni haki yake na hivyo si haki kwa baadhi ya wananchi wa kijiji cha homboza, kunyimwa haki ya kuchagua kiongozi wanayemtaka katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika hivi karibuni.

Mkuu wa wilaya ya Kisarawe  Bi Subira Khamis Mgalu  amewataka wananchi wanaokidhi vigezo kutumia haki yao ya kikatiba kujitokeza na kujiandikisha kwa wingi wakati wa uandikishaji kwenye daftari la wapiga kura na siku ya kupiga kura wajitokeze kwa wingi ili kuwachagua viongozi wanao wataka bila bughudha yoyote.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. TWILA KAMBANGWAApril 16, 2015

    kweli kabisa bi subira wape elimu hao waukae maana wanapoelekea ni pabaya bila yao wenyewe kujua, vilihi waukae mowasa?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...