Klabu ya
michezo ya riadha ya Dar Es Salaam “Dar Running Club” (DRC) imeandaa mashindano ya
mbio yajulikananyo kama “Mayday marathon” yatakayofanyika tarehe 02
Mei 2015 yatakayoanza na kumalizika katika viwanja
vya Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay (Police Officers Mess).
Mgeni rasmi atakuwa ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Inspekta Generali wa Police Ernest Jumbe Mangu (IGP).
Akizungumza na waandishi wa habari Mlezi wa Klabu ya DRC Mkuu
wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni bwana Camillus Wambura) amesema DRC ni klabu
ambayo ilianzishwa rasmi kutokana na makundi mawili tofauti yenye malengo sawa
kimichezo, yaani Kinondoni police jogging club kutoka Polisi mkoa wa Kinondoni
na Dar Es Salaam Athletic Club yenye washiriki kutoka maeneo mbali mbali ya Dar
Es Salaam wakaamua kuungana na kuwa DRC.
DRC ina madhumuni makubwa
ya kuendeleza michezo ya riadha nchini mpaka nje ya nchi na kuhimiza
afya njema kimwili na kiakili, lakini pamoja na hayo muungano huu wa klabu
unasaidia sana kuimarisha mahusiano kati
ya Polisi na raia, hii inasaidia sana
katika usalama na kukuza na kuendeleza dhana ya Polisi jamii na ulinzi
shirikishi kwa jamii. Aliongezea…
Naye Captain wa DRC bi (Stella Mandago, na mratibu
wa mashindano haya amesema kuwa Mashindano haya yanatarajia kushirikisha
wanamichezo mbalimbali kutoka hapa nchini na
nje ya nchi pia, mashindano haya yatakuwa na washiriki watakao shiriki
katika mbio za kilometa ishirini na moja nukta moja (21.1km) na kilomita kumi
(10.0Km) yakiwa na lengo la kukuza na kuendeleza michezo ya riadha Tanzania na
nje ya nchi ili kuwawezesha wanamichezo kufikia hatua za kimataifa na kuhimiza
maisha yenye afya pia kudumisha mahusiano baina aya police na jamii.
Klabu ya michezo
ya Riadha “Dar Runing Club” inachukua fursa hii kukukaribisha kushiriki mbio hizi zinazotarajiwa
kuanza majira ya saa kumi na mbili asubuhi 12:00 katika viwanja tajwa hapo juu,
aliongezea…..
Kutakuwa na
zawadi kwa washindi kumi wa kwanza kwa wanawake na wanaume kama ifuatavyo kwa
nusu marathoni ya km 21
Mshindi wa
kwanza TZS 1,100,000
Mshindi wa
pili TZS 800,000
Mshindi wa tatu
TZS 600,000
Mshindi wa nne
TZS 350,000
Mshindi wa tano
TZS 300,000
Mshindi wa sita
TZS 250,000
Mshindi wa saba
TZS 200,000
Mshindi wa nane
TZS 1500,000
Mshindi wa tisa
of TZS 100,000
Mshindi wa kumi
of TZS 50,000
Kutakuwa pia na
washindi wa 3 kwa mbio za Km 10 kama ifuatavyo
Mshindi wa
Kwanza TZS 500,000
Mshindi wa
PIli TZS 300,000
Mshindi wa
tatu TZS 200,000
MSHINDI WA NNE(4) DEAL
ReplyDeleteMshindi wa nane (8) naona kiasi ni makosa ya kiuhandishi.
ReplyDelete