Mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu mstaafu, Mh. Edward Lowassa (katikati mwenye kapelo), "akitroti" kukimbia sambamba na mamia ya watu waliojitokeza kwenye matembezi ya kuunga mkono kupiga vita dhidi ya mauaji ya watu wenye Ualbino, yaliyofanyika jana kuanzia Uwanja wa Taifa na kuishia kwenye Viwanja vya TCC Club, Chang'ombe jijini Dar es salaam. Katika hotuba yake mwishoni mwa matembezi hayo ya kilomita 5, Mh. Lowassa alimuomba Rais Jakaya Kikwete, "kumwaga" wino, ili kubariki hukumu ya kifo dhidi ya waliohusika na mauaji ya Albino.
Mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu mstaafu, Mh. Edward Lowassa (katikati) akishiriki matembezi ya kuunga mkono kupiga vita dhidi ya mauaji ya watu wenye Ualbino, yaliyofanyika jana kuanzia Uwanja wa Taifa na kuishia kwenye Viwanja vya TCC Club, Chang'ombe jijini Dar es salaam.Kushoto ni Mbunge wa Ilala, Mh. Mussa Zungu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Haya hayaaaaa...kazi kwao wanaosema mamvi mgonjwa .... huyooo anatroti...mwacheni jamani atimize ndoto ...kura yangu anayo!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...