Mhadhiri wa Chuo Cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere,Shadrack Mwakalila akizungumza na waandishi wa habari  (hawapo pichani) juu ya kozi ya uongozi na maadili ya chuo hicho ,Kushoto ni Mhadhiri Msasidizi wa Chuo Cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere,Amon Katunzi iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka)
 
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

Rais Dk.Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kozi ya uongozi na maadili iliyoanzishwa na Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere itayofanyika Aprili 13.

Akizungumza na waandishi wa habari leo,jijini Dar es Salaam,Mhadhiri w Chuo Kumbukumbu Cha Mwalimu Nyerere,Shadrack Mwakalila,amesema kozi hiyo watasoma kwa muda wa miezi mitatu na itakuwa endelevu.

Mwakalila amesema  kozi hiy ni kujenga watu kuwa na maadili ya kutokana na jinsi alivyowajibika Mwalimu wakati wa uhai wake.

Amesema watu wajitokeze katika kusoma kozi hiyo ambayo itasaidia kuwa viongozi na wenye maadili kutokana na kozi hiyo iliyoandaliwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. mi maoni yangu hiyo kozi ianzishwe vyo vyote kwani chuo cha mwl Nyerere pekee hakiwezi kusaidia watumishi wote kwani uozo umetapakaa kama kansa idara zote

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...