Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu
nchini TFF, Jamal Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa Mwenyekiti wa klabu ya
Young Africans, Yusuf Manji kufuatia timu yake kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya
Vodacom msimu wa 2014/2015.
Katika salamu zake za pongezi,
Malinzi amesema kutwaa Ubingwa wa VPL ni jambo muhimu na sasa wanapaswa kuanza
maaandalizi kwa ajili ya michuano ya kimataifa barani Afrika mwakani.
Klabu ya Young Africans imetwaa
Ubingwa wa Ligi Kuu nchini kwa mara ya 25 (ishirini na tano) jana, baada ya
kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya timu ya Polisi Morogoro katika uwanja
wa Taifa huku ikiwa na michezo miwili mikononi kabla ya ligi kumalizika.
Waziri wa Habari, Vijana Utamuduni na
Michezo, Dr. Fennela Mkangara anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za
kukabidhi Kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Mei 6, 2015 katika mchezo
kati ya Azam FC dhidi ya Young Africans.
VILABU VPL
VYAPIGWA FAINI, WAAMUZI WAFUNGIWA
Ruvu Shooting imepigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa
kuzingatia Kanuni ya 14(9) ya Ligi Kuu kwa kutoingia kwenye vyumba vya
kubadilishia nguo (changing room) katika mechi namba 149 dhidi ya Kagera Sugar
iliyochezwa Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga
Pia Ruvu Shooting
imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa kutoingia vyumbani wakati wa
mapumziko kwenye mechi hiyo. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya
14(13) ya Ligi Kuu.
Stand United imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada
ya washabiki wake kuwatupia chupa za maji wachezaji wa akiba wa timu ya Polisi
Morogoro katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga. Adhabu
hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Kuu.
KUSOMA ZAIDI INGIA HAPA
KUSOMA ZAIDI INGIA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...