Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier,  akipata maelezo kutoka kwa Bw. Said Ngosha Magonya, ambaye ni  Kamishina wa Fedha za Nje kuhusu utaratibu uliopangwa na Tanzania katika Mikutano hii ya majira ya kipupwe.

Mikutano ya Majira  Kipupwe imeanza rasmi  Mjini Washington DC.
Mikutano ya majira ya  Kipupwe imeanza rasmi tarehe 14/4/2015 na kuhudhuriwa na nchi mbalimbali wanachama zaidi ya 188. 

Mikutano hii huudhuriwa na maelfu ya wafanyakazi kutoka serikalini, waandishi wa habari, Mashirika na Taasisi zisizo za kiserikali, Sekta binafsi pamoja na kamati za kifedha.Taasisi hizo kwa pamoja zitajadili maendeleo ya kazi za Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa. 

Tanzania ni nchi wanachama katika Mikutano hiyo.Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya  ndiye kiongozi wa ujumbe kutoka Tanzania na ni Gavana katika mikutano hii, akifuatiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali  Dr. Servacius Likwelile ambaye ni  Gavana msaidizi kwa upande wa Benki ya Dunia (WB), aidha  Gavana wa Benki kuu Prof. Benno Ndulu ni Gavana msaidizi kwa upande wa Shirika la Fedha la Kimataifa(IMF).

Imetolewa na:
Msemaji wa Wizata ya Fedha
Ingiahedi C. Mduma
14/4/2015
Washington DC.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...