Na   Bashir   Yakub.

Wako  watu  wengi  wameathirika  kutokana  na  matendo  yanayotokana  na  uzembe,kutojali  au  makusudi ya madaktari. Wapo  waliopata  vilema    vya muda  kutokana  na  uzembe  huo,  wapo  waliopata  vilema  vya  maisha  na  wapo  waliouliwa  na  madaktari hawa hawa.  

 Ajabu  ni kuwa  ukifanya  tathmini  ya  haraka  utaona kuwa    watu  wote waliopata  madhila    kutoka  kwa  madaktari  huhusisha  madaktari  wa serikali  na  katika  hospitali  za  serikali.  Si   rahisi   kukuta  jambo  la ajabu  la  kitabibu  limehusisha  hospitali  binafsi.  Swali  langu   ni  kuwa,  ewe   Mtanzania  daktari  amekusababishia   tatizo  iwe  ugonjwa  wa kudumu,  ulemavu  wa  muda  au  wa  kudumu,  au  hata  kifo  cha   ndugu  au  jamaa,  umechukua  hatua  gani   baada  ya  tukio hilo  ?.  Umekaa  kimya  ukiwa  umeridhika  au  umekaa  kimya  kwakuwa  hujui  la  kufanya ?.

1.INARUHUSIWA   KUMSHITAKI  DAKTARI  KWA  KUSABABISHA    

 MADHARA   KWA  MGONJWA  WAKATI  WA  TIBA.

Wapo  wanaodhani  kuwa  madaktari  hawashitakiwi kwa  kutomhudumia  vyema  mgonjwa.  Hili    si  kweli  daktari  ni  mtumishi  sawa  na  watumishi  wengine    na  kosa  lolote  la  uzembe,  kutojali  au  makusudi  analofanya  na  kusababisha  madhara  kwa  mgonjwa  sheria  inaruhusu  kumchukulia  hatua    daktari  huyo. Sawa  na  mtumishi  mwingine  akitenda  kosa kazini  anaadhibiwa  ndivyo  ilivyo  kwa  madaktari  pia. Kwa    mujibu  wa  sheria  daktari  amepewa  wajibu  wa  hali  ya  juu  kuhakikisha  anatumia  taaluma  yake,  weledi  na  uadilifu  katika  kutoa  huduma  ya  tiba    na  kuepuka  kabisa  hatua au  namna  yoyote  inayoweza  kuleta   madhara  kwa  mgonjwa. 

 Takwa  hili  kwa  daktari  ni  takwa  la  kisheria  na  wala  si  hiyari. Kwa  hiyo  watu  waelewe  kuwa  suala  la  daktari  kutoa  matibabu   kwa  umakini  ni  lazima.  Kitu   kikiwa  lazima (mandatory)  katika  sheria  maana  yake ni  kuwa  kutofanyika  kwake  hutoa  haki  ya  mtendewa  kushitaki.  Hivyo  ndivyo  ilivyo  kwa  madaktari.  Kwa  namna  yoyote  anapokosa  umakini  katika  kutoa  tiba  basi    ni  ruhusa  kwa  mtendewa  kushitaki. 

 KUSOMA ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...