Baada ya huduma za Kilimo Klub,M-Pesa na M-Pawa zinazotolewa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania kuonyesha mafanikio makubwa ya kutumia mapinduzi ya teknolojia ya simu za mkononi kuleta mabadiliko kwenye jamii,hivi sasa kampuni imejipanga kupeleka na kuboresha huduma za mawasiliano vijijini ili ziweze kuwafikia watanzania wengi.
Hayo  yamebainishwa  na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano Kampuni hiyo,Rosalynn Mworia kufuatia kampuni hiyo pamoja na makampuni mengine yanayotoa huduma za simu nchini TTCL,Tigo na Airtel kusaini mkataba na Mfuko wa Kuendeleza Mawasiliano Vijijini (UCAF) hivi karibuni ambapo itatakiwa kupeleka huduma katika kata 36 vijijini na vilevile imesaini mkataba wa kupeleka huduma za mawasiliano  sehemu za mipakani mwa nchi.
“Mawasiliano ni jambo la msingi katika kuleta mabadiliko na kuendeleza jamii kama ambavyo tumeshuhudi. maisha ya watanzania yamerahisishwa tangu kuboreshwa huduma za mawasiliano hususani kuingia kwa makampuni yanayotoa huduma za mkononi ambayo yamekuwa na ubunifu mkubwa wa huduma za kurahisisha maisha ya kila siku ya wananchi”.Alisema.
Aliongeza kuwa huduma hizi ni muhimu kuwafikia watanzania wote hususani waishio maeneo ya vijijini na ndio maana Vodacom siku zote ambayo mtandao wake unawafikia watanzania wengi na zaidi ya asilimia 45 ya minara yake ikiwa imejengwa maeneo ya vijijini itaendelea kuunga mkono jitihada za serikali za kuboresha mawasiliano ya simu katika huduma za vijijini na kubuni huduma zitakazoweza kuleta mabadiliko vijijini.
 Alizitaja baadhi ya huduma za Kilimo Klub,M-Pawa na M-Pesa zinazotolewa na kampuni hiyo kuwa zinaendelea kuleta mabadiliko makubwa kwenye jamii ya watanzania na kuboresha maisha yao kuwa murua. “Tuna imani huduma hizi na nyingine tutakazoendelea kuzibuni zitaleta mabadiliko kwa watanzania wengi hususani wenye kipato cha chini hususani wakulima na kuwatoa katika hali ya chini na maisha yao kuwa bora zaidi”.Alisisiza.
Hivi Karibuni Naibu Waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika Mh.Godfrey Zambi alisema kuwa huduma zinazolenga kuboresha maisha ya wakulima vijijini  kama ilivyo huduma ya Kilimo Klub ni muhimu sana kwa jamii ya watanzania ambao asilimia kubwa ni wakulima na wanaishi maisha ya vijijini wakiwa na maisha duni kiasi cha kutojitosheleza kwa mahitaji yao muhimu.
Huduma ya kilimo inawawezesha wakulima kupata taarifa mbalimbali kuhusu shughuli zao za ukulima kupitia simu zao za mkononi ambapo vilevile wanaweza kutuma na kupokea fedha,  kufanya mihamala ya malipo kupitia huduma ya M-Pesa na wanaweza kujiwekea akiba na kupata mikopo rahisi na yenye masharti nafuu kupitia huduma ya M-Pawa ya Vodacom kwa kushirikiana na Benki ya CBA ambayo inaendelea kupata umaaruufu mkubwa siku hadi siku
Huduma hii inayolenga kubadilisha maisha ya mamilioni ya watanzania inatolewa na Vodacom pekee kwa kushirikiana na taasisi za , Olam International, Connected Farmers Alliance na Techno Serve .
 Ofisa Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Georgia Mutagahywa  (wa pili kutoka kulia) akisaini mkataba wa miradi miwili ya upelekaji mawasiliano vijijini awamu ya 2A kati ya Mfuko Wa Mawasiliano Kwa Wote (UCSAF)na kampuni za simu za mkononi katika hafla iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Miradi hiyo ni upelekaji wa mawasiliano mipakani na maeneo maalum na mradi wa kuunganisha Intaneti kwenye Shule za Umma,wengine ni  mwakilishi wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania (wa kwanza kulia), Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya simu za mkononi ya MIC Tanzania (Tigo) Cecilia Tiano (wa pili kutoka kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko Wa Mawasiliano Kwa Wote (UCSAF) Eng. Peter Ulanga (wa tatu kulia)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...