Na Veronica Mheta, Arusha

WAKANDARASI wameaswa kuacha tabia ya kujenga majengo ya serikali pamoja na wananchi chini ya viwango kwalengo la kupata faida kubwa na kuleta hasara kubwa katika nchi.

Aidha serikali inafanya kila linalowezekana ili kulipa madeni ya wakandarasi wazalendo ikiwemo kupata mikopo ya riba nafuu kwaajili ya kuwezesha wakandarasi kupata zabuni za ujenzi wa majengo makubwa zaidi yanayojengwa na wageni kutoka nchi za nje.

Kauli hiyo ilitolewa jana Jijini hapa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Mussa Iyombe wakati alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa nne wa mwaka wa Chama cha Makandarasi Wazalendo Tanzania (ACCT) unaofanyika kwa siku mbili .

Alisema si vyema wakandarasi kufanya kazi kwa kutaka faida kubwa na kupelekea hasara kwa wananchi pamoja na serikali kwani ufanyaji kazi kwa kulipua unashusha heshima katika fani hiyo sambamba na kuleta hasara kwa serikali kwani baadhi ya majengo yanajengwa chini ya viwango.

Pia alisema hivi sasa serikali imefanya mazungumzo na Gavana wa Benki Kuu (BoT) kwaajili ya kuwasaidia wakandarasi waweze kupata mikopo yenye riba nafuu kutoka serikalini itakayowasaidia kupata fedha na kujenga majengo makubwa zaidi badala ya wageni kutoka nje ya nchi kupata zabuni za kujenga majengo hayo huku wakandarasi wazalengo wakiambulia asilimia 40 tu ya ujenzi.

“Naomba msibabaike na faida kubwa na kuleta hasara kwa Taifa angalieni uzalendo lakini najua mnaidai serikali fedha nyingi ila tuko mbioni kuwalipa madeni yenu na pia hivi sasa serikali itatoa mikopo yenye unafuu ili muweze kujenga majengo makubwa ya kisasa badala ya wageni kujenga maana wakipata faida wanarudisha kwao huku wakandarasi wazalendo wakiambulia kazi za matengenezo madogo madogo”.

Naye Mwenyekiti wa ACCT, Mhandisi Milton Nyerere alisema kuwa chama hicho kipo katika hatua ya kuanzisha chuo cha ufundi kwaajili ya kukuza uwezo kwa kuendesha mafunzo ya fani mbalimbali za kikandarasi kwa mafundi wa makampuni ya makandarasi ili kupunguza changamoto ya wataalam wanayokumbana nayo kwenye utekelezaji wa miradi.

Aliongeza kuwa chama hicho kinajumla ya wanachama 78 na kimekuwa na mahusiano mazuri na Bodi ya Wakandarasi (CRB)na wadau mbalimbali katika uimarishaji wa ubora wa kazi sambamba na kuanzisha taasisi ya fedha benki kwaajili ya makandarasi wazalendo ili kuwasaidia kupambana na changamoto ya mitaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. TATIZO LA HAWA WAKANDARASI WA KIBONGO SEHEMU YA KUWEKA CEMENT MIFUKO 100 WAO WANAWEKA MIFUKO 30 TU ALAFU PESA WANATIA NDANI, NCHI HII UFISADI KILA KONA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...