Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa pamoja na viongozi wa elimu nchini watembelea Singapore kujifunza jinsi nchi hiyo ilivyofanya mageuzi makubwa katika mfumo wa elimu na mafunzo.
Mfumo wa elimu wa nchi hiyo, unalenga kuendeleza wanafunzi katika kuwapatia stadi muhimu zinazohitajika kwa maendeleo ya nchi.
Mfumo wa elimu wa nchi hiyo, umeweka mkazo zaidi katika kutoa mafunzo ya ufundi stadi ambayo yanatoa ujuzi kwa mhitimu kuweza kufanya kazi katika kada ya kati.
Takwimu za elimu zinaonyesha kuwa, asilimia 29.4 ya wahitimu wanajiunga na vyuo vikuu; asilimia 28.2 wanajiunga na vyuo vya elimu ya ufundi na asilimia 46.4 wanajiunga na vyuo vya utaalamu mbalimbali (Polytechnic).
Katika ziara hiyo Dkt Kawambwa na ujumbe wake walipata nafasi ya kutembelea chuo kikuu cha Taifa cha Singapore (National University of Singapore), Chuo cha Elimu ya Ufundi (Institute of Technical Education) na Chuo cha Ufundi stadi (Republic Polytechnic) ambapo katika vyuo hivyo walipata nafasi ya kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa na wanafunzi pamoja na walimu.
Waziri wa Elimu na Mafunzo Dkt Shukuru Kawambwa akielezea Jambo katika Mkutano kati ya viongozi wa elimu kutoka wa Tanzania na Viongozi wa Wizara ya Elimu ya nchini Singapore.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...