Meneja Biashara wa Idara ya Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Grace Lyon akiwapa elimu kuhusiana na matumizi ya vitambaa vya hedhi baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi iliyopo Hydom Mkoa wa Manyara.Vodacom Foundation kupitia mradi wake wa Girl Pawa imelenga kuwawezesha wasichana  kutimiza ndoto za maisha yao kwa kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowafanya  wasibaki nyuma katika masomo, kutojiamini na utoro mashuleni wanapokuwa kwenye vipindi vya hedhi.Mradi huu  ambao unatekelezwa  na taasisi ya T-MARC wakishirikiana na USAID pamoja na Vodacom Foundation leo zimeungana na mataifa mengine katika  kuadhimisha siku ya hedhi duniani.

Changamoto mbalimbali zinazowakabili wasichana wanapokuwa kwenye vipindi vya hedhi yanapaswa kujadiliwa na kutafutiwa ufumbuzi wa kudumu kwa kuwa yanachangia kurudisha nyuma jitihada za kuwainua watoto wa kike nchini.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia ikiwa leo ni maadhimisho ya siku ya hedhi duniani ambapo Vodacom Foundation, imekuwa mstari wa mbele kupambana na changamoto zinazowakabili watoto wa kike nchini ikiwemo kusaidia wasichana vifaa vya kuwaweka salama  wanapokuwa kwenye vipindi vya hedhi kupitia mradi wake wa Girl Pawa wenye kauli mbiu isemayo “Hakuna Wasichoweza”.
 “Vodacom Foundation kupitia mradi wake wa Girl Pawa imelenga kuwawezesha wasichana  kutimiza ndoto za maisha yao kwa kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowafanya  wabaki nyuma baadhi yake zikiwa ni ukosefu wa elimu , kutojiamini na utoro mashuleni wanapokuwa kwenye vipindi vya hedhi.Mradi huu  ambao unatekelezwa  na taasisi ya T-MARC  umeonyesha mafanikio katika awamu ya kwanza.”Alisema.
Mworia alisema lengo la mradi wa “Hakuna Wasichoweza”  ni kuwapatia elimu ya uzazi, afya, kuwajengea uwezo wa kujiamini na kuwapatia Pedi za gharama nafuu watoto wa kike waliopo katika umri wa kuvunja ungo na umeanza kutekelezwa mkoani Mtwara lengo likiwa ni kutekelezwa katika mikoa mbalimbali ya Tanzania katika siku za usoni.
Meneja wa mradi huu wa T-MARC,Doris Chalambo amesema tangu mradi huu uanze kutekelezwa  idadi ya wasichana wanaohudhuria masomo mashuleni imeongezeka tofauti na siku za nyuma ambapo wasichana walipokuwa wanaingia katika hedhi wengi wao walikuwa wanashindwa kuhudhuria kwenye masomo kutokana na kutokuwepo na mazingira rafiki ya kukabiliana na hali hiyo 
Kutokana na mafanikio yaliyopatikana katika awamu ya kwanza ya mradi wa kuwawezesha wasichana kupitia mradi wa Hakuna  Wasichoweza, taasisi ya Vodacom Foundation imeongeza ufadhili wa Dola za Kimarekani 166,000 katika awamu ya pili ili mradi uendelee na uweze kuwafikia wasichana wengine wapatao 4,200 katika shule nyingine 10 katika mkoa wa Mtwara.
Awamu ya kwanza ya mradi huu ilifadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Watu wa Marekani (USAID) ambalo lilitoa ufadhili wa Dola za Kimarekani 200,000 na taasisi ya Vodacom Foundation ambayo ilitoa Dola za Kimarekani 100,000 na umenufaisha zaidi ya wasichana  5,000 ambapo katika awamu ya pili unategemewa kunufaisha wasichana wengi zaidi.
Serikali nayo imetangaza kulivalia njuga tatizo hili ambapo hivi karibuni imesema kuwa itaboresha mazingira kwenye shule zake ili yawe rafiki kwa wasichana wanapokuwa kwenye hedhi ili kupunguza utoro mashuleni.Kauli mbiu ya siku ya hedhi duniani mwaka huu ni “Usisite Kuzungumzia Hedhi”.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...