Mwenyekiti wa Posta na Simu SACCOS, Bw. Lawrence Mwasikili (katikati) akisisitiza jambo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuanza kuuzwa kwa viwanja 1,500 vilivyoko Msata, wilaya ya Bagamoyo kwa wanachama wake.  Walioambatana naye katika mkutano huo wa waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam ni Afisa Mkuu Mtendaji wa Ushirika huo, Bw. Deogratias Ngalawa (kushoto) na Afisa Tawala, Bw. Jeremiah Miselya.
 Afisa Mkuu Mtendaji wa Posta na Simu SACCOS, Bw. Deogratias Ngalawa akisisitiza jambo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuanza kuuzwa kwa viwanja 1,500 vilivyoko Msata, wilaya ya Bagamoyo kwa wanachama wake.  Wengine walioambatana naye katika mkutano huo wa waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam ni Mwenyekiti wa Ushirika huo, Bw. Lawrence Mwasikili (katikati) na Afisa Tawala, Bw. Jeremiah Miselya (kulia).


Posta na Simu Saccos Ltd imewaalika wanachama wake kununua   viwanja vilivyopimwa Msata, wilaya ya Bagamoyo  kuanzia jana hadi  tarehe 31 Mei, 2015 ili wajenge nyumba bora au watume hati za viwanja  kupata mikopo mikubwa.
Akitangaza uamuzi wa ushirika huu jana Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wake, Bw Lawrence Mwasikili,   amesema kuwa viwanja  viko katika makundi matatu na bei zake ni tofauti.  Viwanja vya maeneo madogo ni 870 na kila kiwanja kinagharimu milioni 2; ukubwa wa kati ni viwanja 465 na kiwanja kitapatikana kwa milioni 3.5.  Viwanja ya maeneo makubwa ni 165 na kila kiwanja ni milioni 5.
Amesema kuwa kwa wanachama  fedha ya kumilikishwa viwanja itakatwa kwenye mishahara yao kwa miaka miwili.
Bw Mwasikili amewahakikishia wanachama kuwa upimaji wa viwanja hivyo umethibitishwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, na kueleza kuwa wanachama lazima waombe umiliki wa viwanja hivyo katika kipindi kilichowekwa kwani baada ya 31 Mei, 2015, watu wasiokuwa wanachama wataalikwa kumiliki viwanja hivyo kwa utaratibu kununua mita ya mraba kwa shilingi 4,500.
Amesema kuwa uamuzi huu unatokana na ukweli kwamba wanachama wa ushirika huu wengi wana nyumba katika maeneo yasiyopimwa na kwa hiyo hawawezi kupata mikopo.
 Akisisitiza umuhimu wa wanachama kuchukua viwanja kwa utaratibu wa upendeleo katika muda  uliotengwa, Mwenyekiti alisema “tutawaalika wananchi wa kawaida kuchukua viwanja hivi kuanzia Juni mosi, mwaka huu.” Wananchi  wapata viwanja kwa kulipa fedha taslimu mara moja  au kwa mikupuo itakayoidhinishwa.
Katika mkutano huo,  Ofisa Mkuu (CEO)wa ushirika  huu,Bw. Deogratias Ngalawa, aliwambia waandishi wa habari kuwa   wanachama wachangamkie fursa hiyo kwa vile viwanja   vitapatikana  kwa gharama ndogo ikilinganishwa na gharama za viwanja vilivyopimwa vya  taasisi nyingine.
Alisema ushirika wao umkopesha mwanachama hdi milioni 25 na kwa kuwa kuna wanachama wanohitaji mikopo mikubwa hati za viwanja hivi zitawasaidia kupata mikopo watakayoomba.
Wanachama wa Posta na Simu Saccos ni wafanyakazi  wa  Shirika la Posta Tanzania, Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Tanzania Postal Bank (TPB) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCCRA).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...