Bw. Sam Kutessa, Rais  wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Na  Mwandishi Maalum, 
New York 
Jumuiya ya Kimataifa  inajiaanda  kwa  mkutano maalum na  wa aina yake kufanyika, ambapo  nchi wanachama watakutana  na  kujadiliana kwa kina kuhusu  changamoto na adhari kubwa  zitokanazo na  biashara haramu na matumizi ya dawa za kulevya.
 Mapema wiki iliyopita,    wajumbe wanaoziwakilisha nchi  zao  hapa  Umoja wa Mataifa, walikuwa na mkutano wa siku moja ambao ulikuwa ni sehemu ya maandalizi ya mkutano huo maalum utakaofanyika mwezi Aprili  2016.
Mkutano huo wa maandalizi uliofanyika hapa  Umoja wa Mataifa na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwamo mawaziri kadhaa kutoka nchi hasa  za  Amerika ya Kati ambako   nchi nyingi zinakabiliwa  na changamoto kubwa ya  biashara hiyo, uliandaliwa na Bw. Sam Kutessa, Rais  wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Katika  majadiliano ya  mkutano huo ,  ilidhihirika wazi kwamba hakuna nchi hata moja   duniani  iwe tajiri au maskini ambayo  haijakumbwa  na  janga  la biashara na  matumizi ya dawa za kulevya.
“ Hakuna nchi ambayo imepona kutokana na biashara hii yenye thamani  ya mabilioni  ya dola. Licha ya juhudi kubwa na raslimali nyingi ambazo mataifa yanatumia   kukabiliana na janga hili, lakini tatizo  linaendelea kukua” akasema Bw. Sam Kutessa wakati akifungua mkutano huo. Kwa habari kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...