Siku 8 zimebaki kufikia kilele cha tuzo za filamu mwaka 2015.

Ikiwa zimebaki siku chache kufikia kilele cha tuzo za filamu kwa mwaka huu ambapo Tuzo za Filamu Tanzania (TAFA) zinafanyika kwa mara ya kwanza nchini Mei 23, 2015 Mwalimu Nyerere International Conference Center jijini Dar es Salaam. 

Haya ni mapinduzi makubwa katika tasnia ya filamu nchini kwani ni kuonesha mafanikio. Ni vipengele mbalimbali vilivyopo katika kinyang’anyiro cha tuzo za filamu mwaka huu 2015. Tuzo hizo ambazo ni kubwa na zenye hadhi ya juu zimeandaliwa na Shirikisho la Filamu Tanzania na washirika mbalimbali .

 “Kazi kubwa ya Shirikisho la Filamu Tanzania ni kusaidia kukuza tasnia ya filamu na kuunga mkono jitihada za wasanii kwa namna mbalimbali. Mbali na hilo pia ni daraja linalowaunganisha wasanii wa tasnia ya filamu na Bodi ya Filamu nchini hivyo kurahisisha utendaji wa kazi zao. 

Ninayo kamati ya maandalizi iliyo imara na thabiti ambayo imefanya kazi katika mazingira magumu usiku na mchana kuhakikisha tunapata halfa nzuri na ya namna yake ambayo haijawahi kutokea”, Alisema Simon Mwakifwamba, Raisi wa Shirikisho la Filamu Tanzania.

Aliongeza kwa kusema kuwa tasnia ya filamu nchini bado ina safari ndefu ukilinganisha na Hollywood ambao wameshapiga hatua kubwa. Tuzo hizi sasa ni jambo wanapaswa kujivunia kwa wasanii na watengeneza filamu kujivunia. 

Imeripotiwa kuwa tasnia ya filamu imechangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa pato la taifa hili linathibitishwa na taarifa ya mapato nchini ya hivi karibuni, na hili linadhihirisha kuwa tasnia ya filamu inafanya kazi kubwa ya kupunguza tatizo la ajira nchini ambalo limekua ni tatizo kwa vijana wengi hapa nchini.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...