WOTE TUNATAKA KUSOMA HADI CHUO KIKUU! Ndivyo wanavyosema wanafunzi wa Shule ya Msingi Uhuru mjini Dodoma baada ya kuulizwa nani kati yao angependa kusoma hadi chuo kikuu na Ofisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bi. Veneranda Malima (kulia) jana (Jumanne, Mei 12, 2015). Wanafunzi hao na walimu wao walitembelea banda la HESLB ambayo inashiriki katika maonesho ya Wiki ya Elimu yanayaoendelea katika viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru mjini Dodoma Bi. Conces Shirima akisaini kitabu cha wageni cha Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) wakati alipotembelea banda la HESLB katika maonesho ya Wiki ya Elimu yanayaoendelea katika viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Cosmas Mwaisobwa akibadilishana mawazo na Dkt. Jacob Chembele wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kuhusu urejeshaji wa mikopo inayotolewa na HESLB. Dkt. Chembele alitembelea banda la HESLB ambayo inashiriki katika maonesho ya Wiki ya Elimu yanayaoendelea katika viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma.
Ofisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bi. Veneranda Malima (kulia) akiongea na wanafunzi wa Shule ya Msingi Uhuru mjini Dodoma wakiwa na Mwalimu wao Bw. Ikutto Bakari (katikati). Wamafuzni hao walitembelea banda la HESLB ambayo inashiriki katika maonesho ya Wiki ya Elimu yanayaoendelea katika viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma. (Picha na HESLB)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...