Majenerali wawili waliotekeleza jaribio la mapinduzi nchini Burundi dhidi ya rais Pierre Nkurunziza wametiwa mbaroni baada kushidwa kwa jaribio lao hilo, huku kiongozi mkuu wa mapinduzi hayo jenerali Godefroid Niyombare akidaiwa kuingia mititi na sasa anasakwa.

Hayo yemeelezwa leo hii na Msemaji wa Rais Nkurunziza,Willy Nyamitwe.

Awali Jenerali Niyombare alikaririwa akikiambia chombo cha habari cha AFP kwamba yeye na wafuasi wake watajisalimisha kwa serikali ya Rais Nkurunziza, huku akiongezea kuwa ''natumai hawatatuua''.
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza
Naibu kiongozi wa jaribio la mapinduzi nchini Burundi, alikiri kuwa jaribio lao limeshindwa kufanikiwa, baada ya kukabiliana na upinzani mkali kutoka kwa jeshi la taifa hilo. Habari za kushindwa huko zimetolewa wakati rais Pierre Nkurunziza akitangaza kuwa amerejea nchini Burundi.

Akitangaza kupitia ukurasa wake wa Twitter, Nkurunziza aliwashukuru wanajeshi na polisi kwa ''uzalendo wao'', na wananchi wa Burundi kwa ''subira'' waliyoidhihirisha.

Majaribio ya kuiangusha serikali ya rais Pierre Nkurunziza yalitokea yeye akiwa nchini Tanzania, alikokuwa amekwenda kuhudhuria mkutano wa marais wa kikanda kuhusu hali ya kisiasa nchini mwake.
Kiongozi mkuu wa Jaribio la Mapindizi nchini Burundi,Meja Jenerali Godifroid Niyombare
Lakini mpaka wakati huu, haijulikani hasa wapi alipo rais huyo, na taarifa za kurejea kwake hazikuthibitishwa na vyanzo huru.

Kufuatia mkutano wa dharura jana Alhamisi, Baraza la amani na usalama la Umoja wa Afrika, lililaani jaribio lolote la kutwaa madaraka kupitia vurugu nchini Burundi, na kuhimiza mazungumzo kati ya makundi yanayohasimiana.

Mjini New York, Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon na maafisa wake waandamizi, walikuwa wanafuatilia matukio nchini Burundi kwa wasiwasi mkubwa, alisema msemaji wake.

Nalo Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeonya kuwa litawachukulia hatua wale wote wanaowafanyia vurugu raia na kutaka kurejeshwa haraka kwa utawala wa sheria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 15, 2015

    Hii ni hatua nzuri, hakuna sababu ya vita wala wananchi kuuana Burundi. Waliosababisha jaribio la mapinduzi wajibu mashitaka kwa mujibu wa sheria, Burundi ikae kwa amani na utengamano. Funzo ni vijana wacha kushabikia vita yoyote inaahthiri sio nzuri.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...