Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (kushoto),
akizungumza na Kamishna wa Forodha na Ulinzi wa Mipaka toka Serikali ya Marekani
Bw. R. Gil Kerlikowske alipomtembelea ofisini kwake kuzungumzia masuala ya
ushirikiano wa shughuli za kiulinzi kati ya Serikali ya Tanzania na Marekani. Kulia ni
Msaidizi wa Balozi wa Marekani hapa nchini Bi. Virginia Blaser.
Kamishna wa Forodha na Ulinzi wa Mipaka toka Serikali ya Marekani Bw. R. Gil
Kerlikowske (kulia), akifafanua jambo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe.
Mathias Chikawe wakati wa mazungumzo yaliyofanyika Ofisini kwa Waziri Chikawe
kuhusu kuimarisha ushirikiano wa masuala ya kiulinzi kati ya Serikali ya Tanzania na
Marekani.
Ujumbe kutoka Serikali ya Marekani wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Mhe. Mathias Chikawe alipokuwa akizungumza nao wakati walipotembelea Ofisini kwa
Waziri Chikawe. Ujumbe huo uliongozana na Kamishna wa Forodha na Ulinzi wa
Mipaka toka Serikali ya Marekani Bw. R. Gil Kerlikowske.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mathias Chikawe (kulia), akizungumza na
Kamishna wa Forodha na Ulinzi wa Mipaka toka Serikali ya Marekani Bw. R.Gil
Kerlikowske (katikati) wakati akiondoka mara baada ya kumaliza mazungumzo yao
Ofisini kwa Waziri Chikawe. Kushoto ni Msaidizi wa Balozi wa Marekani hapa nchini Bi.
Virginia Blaser.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...