Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini - TFF, Jamal Malinzi amewatakia kila la kheri Wawakilishi pekee wa Tanzania katika Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CC) timuYoung Africans katika mchezo wake wa marudiano dhidi ya timu ya Etoile du Sahel utakaochezwa kesho nchini Tunisia.

Katika salamu zake Malinzi amesema ,Young Africans wakiwa ndio timu wawakilishi pekee wa Tanzania na Afrika Mashariki katika michuano ya kimataifa barani Afrika wanapaswa kupambana kuhakikisha wanasonga mbele katia hatua inayofuata.

Katika mchezo wa awali uliofanyika wiki mbili zilizopita jijini Dar es salaam, Young Africans ilitoka sare ya bao 1- 1 na Etoile du Sahel, na mshindi wa jumla kwa mchezo wa huo, atacheza hatua ya mtoano (Play-off) dhidi ya timu zitakazokuwa zimetolewa kwenye Ligi ya Mabingwa (CL) kuwania kufuzu kwa hatua ya makundi.

Mchezo huo wa marudiano utapigwa kesho jumamosi katika dimba la Olympique de Sousse katika mji wa Sousse kuanzia majra ya saa 3 kamili usiku kwa saa za Afrika Mashariki na Kati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...