MWL. ERNEST MWAMKAI KIONDO

Mpendwa Baba, tarehe 22 May 2015 umetimiza mwaka mmoja tangu ututoke hapa duniani kwa mapenzi yake Mwenyezi Mungu.

Tunakukumbuka sana kwa malezi, upendo na ushauri wako  ambao daima ndio dira yetu na kumbukumbu yetu.

Unakumbukwa sana na Wazazi wenza Mama Anna na Mama Agatha, Dada zako na sisi wanao, wakwe zako, wajukuu wote pamoja na ukoo wote wa Kiondo, Bendera, Mbaruku, Msangazi, Bila, Mjata na  Nyangasa.

Japo haupo tena pamoja nasi kimwili, lakini kiroho tuko pamoja nawe kila siku.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu aendelee kukuhifadhi  mahali pema peponi.

AMEN.

Kutakuwa na misa ya kumuombea Marehemu Mzee wetu Jumamosi  tarehe 6/6/2015 katika Kanisa la Mtakatifu Yohana  Krisostomo, Majani Mapana, Tanga.

Misa inategemewa kuanza saa 3 asubuhi na kabla ya hapo, Ijumaa tarehe 5/6/2015 kutakuwa na mkesha  nyumbani kwa Marehemu Kwaminchi Tanga, karibu na Uwanja wa saba saba.
Karibuni sana.

MPENDWA BABA TUTAKUKUMBUKA DAIMA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...