Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Maalim Seif Sharif Hamad amewataka Wazinzibari kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura linalotarajiwa kuanza Mei 16 mwaka huu, ili waweze kutumia haki zao  kikatiba za kushiriki uchaguzi mkuu kwa kupiga kura.

Maalim Seif Sharif Hamad ambaye ni Katibu Mkuu wa Chama Cha  Wananchi (CUF),amesema kuwa uchaguzi mkuu uliopita ulikuwa wa uhuru na wa amani lakini ulikuwa na kasoro katika daftari la wapiga kura, kwamba wapiga kura walikuwa na kadi mbili hali ambayo kwa sasa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) inapaswa kuliangalia jambo hilo kwa umakini.

Amesema kuwa katika kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu  Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ipitie upya wapiga kura kwa kutumia mfumo wa kieletroniki kuhakiki makosa yaliyokuwa yakijitokeza kwa watu kujiandikisha mara mbili.

Maalim Seif amesema kuwa katika kasoro hizo ZEC iharakishe kutangaza majimbo ya uchaguzi kutokana na kazi hiyo ilishafanywa muda mrefu kupitia Wizara ya  Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ.

Amesema katika kasoro zilizokuwemo kwenye daftari la wapiga kura ni pamoja watu waliofariki kuendelea kupiga kura kutokana na mfumo  huo wa kutohakiki wapiga  kura pamoja na watu wasio wakazi wa Zanzibar kupiga kura.

Hata hiyo amesema kuwa atagombea katika uchaguzi mkuu na yaye ana sifa na wengine wenye sifa wanaweza kuomba ridhaa ndani ya chama kugombea .


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na Waandishi wa habari katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo,juu ya harakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu Zanzibar, kulia ni Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano ya Umma, Salim Biman na kushoto ni Naibu katibu Mkuu Zanzibar (CUF),Nassoro Ahmed Mazrui.

Mkurugenzi wa mambo ya Nje wa CUF Ismail Jussa, akijibu maswali mbalimbali yaliyoulizwa na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika leo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa kitengo cha Sera,Utafiti na Mafunzo, Hassan Jani Masoud akielezea  juu ya utafiti walioufanya kupitia kitengo hicho cha CUF juu ya changamoto ya daftari la wapiga kura Zanzibar katika mkutano uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya waandishi habari wailiohudhuria katika mkutano na ulioitishwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Maalim Seif Sharif Hamad ,(PICHA NA EMMANUEL MASSAKA,GLOBU YA JAMII).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...