Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

 CHAMA cha Wanawake Wanasheria Tanzania (TAWLA) wamefanya maadhimisho  ya miaka 25 ya kujenga uwezo  na  kufanya uchechemuzi juu ya  haki za  wanawake, tangu kuanzishwa kwake mwaka 1990 hapa nchini.

 Akizungumza katika uzinduzi wa Maadhimisho ya Chama hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa jengo la  YWCA jijini Dar es Salaam leo,  Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wanasheria (TAWLA), Magreti Ringo amesema kuwa  chama hicho kimefanikiwa kutoa msaada wa kisheria kwa wanawake wasiopungua milioni tano kupitia vituo vilivyopo Dar es Salaam,Tanga,Arusha na Dodoma.

 Pia chama hicho kimefanikiwa kutoa mafunzo kwa wasaidizi wa kisheria 402 ili kuhakikisha jamii  inapata msaada wa kisheria na kuhamasisha jamii, kujua masuala ya kisheria kupitia machapisho mbalimbali.

 Ringo amesema kuwa  chama chicho  kinaratibu  muungano wa  jukwaa la jinsia la katiba, ambalo limefanya kazi na kuchangia kuwepo kwa ibara nyeti zinazolinda haki za kijinsia kwenye katiba inayopendekezwa.

 Katika maadhimisho ya miaka 25 ya chama hicho kimehamasisha uandikaji wa wosia bila gharama yeyote.

 Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wanasheria (TAWLA), Magreti Ringo akizungumza na wandishi katika maadhimisho ya miaka 25 ya Chama cha Wanawake Wanasheria Tanzania (TAWLA) leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Mkurugenzi wa chama hicho,Tika Mwambipile na kushoto ni Mjumbe wa Baraza uuguzi wa TAWLA,Annamaria Moreybo.

 Baadhi ya waandishi wa Habari waliohudhuria katika uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 25 ya  Chama cha Wanawake Wanasheria Tanzania (TAWLA).(Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...