Na  Bashir  Yakub.

Makampuni  ya  simu  kama  Vodacon, Airtel, Tigo, Zantel, Sasatel, na  mengineyo  yamekuwa  yakitenda  makosa  mbalimbali  kwa wateja  wao.  Mara  kwa  mara  wateja  wa  simu  wamekuwa  wakilalamikia  matendo  ya  makampuni   haya  lakini  wengi  wao  wamekuwa  hawachukui  hatua  zaidi  ya  kulalamika. Ni  watu  wachache  mno  ambao  wamekwishachukua  hatua  za  kisheria  dhidi  ya  makampuni  haya licha  ya  uonevu  mkubwa wa   kihuduma   wanaousababisha.   Ukiangalia  kwa  haraka  utaona  kuwa walio  wengi  hushindwa  kuchukua  hatua   kwanza  kwa  kutojua  kama    kuna  uwezekano  wa  kuchukua  hatua , pili  kutokujua  kama  kilichotendeka  ni kosa  na  kinahitaji  adhabu  au  wakati  mwingine  kwa  kuamua  kuacha  tu. 

1.MNIGERIA  ALIPWA  USD  90,000 KWA  KOSA  LA  KAMPUNI  YA  SIMU.

Nchi  kama  marekani,  uingereza  na  karibia  nchi  nyingine  za  ulaya  zote,  na  Afrika  zaidi  Nigeria  na  Afrika  kusini  makampuni ya  simu  yamekuwa  yakilazimika  kulipa  fidia  nyingi mara  kwa  mara  kwa  wateja  wao  kutokana  na  makosa mbalimbali  ambayo    makampuni  yamesababisha  kwa  wateja.  Hivi  karibuni  nchini  Nigeria  kampuni    moja  ya  simu  imelazimika  kumlipa  fidia  ya USD  90,000  mtu  mmoja  ajulikanaye  kwa  jina  la Edo  Emeka  baada  kuishtaki  kampuni  hiyo  kwa  kumfungia  kadi/namba(line)  yake  pasi  na  sababu  za  msingi. 

 Katika  kesi  hiyo  mlalamikaji  Emeka  aliieleza mahakama  kuu  mjini  Lagos  usumbufu  alioupata  kwa   kitendo  hicho  cha  kufungiwa  namba  yake  kitendo  kilichopelekea  mahakama  iamuru  alipwe tuzo(decree)  hiyo.  Aidha  zipo  kesi  nyingi  katika  nchi  mbalimbali  ambapo  watu  wamelipwa   mamilioni  ya  pesa  kutokana    na  makosa   yanayosababishwa  na  makampuni  haya. Hapa  kwetu  makampuni haya  hutengeneza  faida  tu   na  sisi hatuyawajibishi  kwa namna  yoyote  kwa  makosa   na usumbufu tunayosababishiwa  kila  siku.

2.   KWA  MAKOSA  HAYA  WAWEZA KUISHTAKI  KAMPUNI  YA  SIMU.

Hapa  kwetu  sawa  na  nchi  nyingine  duniani   makosa  ya makampuni  ya  simu  kwa  wateja  wao  hufanana. Kuna kufunga  namba  ya  mtu  bila  sababu  za  msingi,  kukata  salio  la  mtu    bila  sababu  za  msingi, kumwekea  mtu    mwito  wa simu  ambao  yeye  mwenyewe  hajachagua , kutumia  mziki  wa  msanii  katika  program  yoyote   bila  ridhaa  yake , kutokuwa  hewani  au  kukata  mawasiliano  bila  taarifa  kwa  wateja,  majenereta  ya  minara kusabababisha usumbufu  na  kelele  kwenye  makazi  ya  watu,  kwa kutaja  ni machache.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...