Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitia saini kwenye kitabu cha kumbukumbu ya Marehemu John Nyerere, mtoto wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili tarehe 9.5.2015. Shughuli ya kuaga mwili wa marehemu John imefanyika nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere huko Msasani jijini Dar es Salaam leo.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiteta jambo na Mama Maria Nyerere mara baada ya shughuli ya kuaga mwili wa Marehemu John Nyerere huko Msasani jijini Dar es Salaam, Marehemu John anatarajiwa kuzikwa Aprili 13, katika kijiji cha Butiama,Mkoani Mara.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa pamoja na Mama Maria Nyerere na Mama Fatma Karume (wa nne kutoka kushoto) pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha-Rose Migiro wamesimama mbele ya jeneza wakati wa shughuli ya kuaga mwili wa Marehemu John Nyerere iliyofanyika Msasani jijini Dar es Salaam,Mwili wa Marehemu John unatarajiwa kusafirishwa kesho kwenda Butiama  mkoani Mara kwa mazishi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...