Mpiga Picha maarufu nchini, Albert Manifester, Mei 24 mwaka huu alifanya maonyesho ya baadhi ya picha alizopiga ikiwa ni sehemu ya kazi zake na baadhi ya picha zilizouzwa siku hiyo zilifanikisha kupatikana kwa kiasi cha shilingi milioni kumi na laki Tatu ambapo asilimia 50 ya mauzo hayo yalitolewa ili kusaidia huduma ya afya ya uzazi katika kijiji cha Kipamba kinachoishi watu wa jamii ya Wahadzabe.

Akizungumza katika hafla hiyo, Manifester alisema kuwa "picha inaongea haraka zaidi kuliko maneno, hivyo na amini kupitia jicho langu nitabadilisha maisha ya watanzania wengi, naanza na watanzania wenzetu Wahadzabe kuboresha huduma ya afya ya uzazi kwa wakina mama".
Mgeni rasmi katika hafla ya maonyesho ya picha zilizopigwa na Albert Manifester (kushoto), Mama Mwantum Malale (kulia) akipokea moja ya picha kama zawadi kutoka kwa mpiga picha huyo.
Mpiga Picha maarufu, Albert Manifester (kushoto) akionyesha sehemu ya kazi zake kwa Mgeni rasmi katika hafla hiyo ya maonyesho ya picha, Mama Mwantum Malale wakati alipokuwa akitembelea shemu mbali mbali kuona picha hizo. Hafla hii ilifanyika kwenye hoteli ya Hyatt Regency, Jijini Dar es salaam.
Mpiga Picha maarufu, Albert Manifester (kushoto) akiwaeleza jambo, Mgeni rasmi katika hafla hiyo ya maonyesho ya picha, Mama Mwantum Malale pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Mh. Edward Ole Lenga wakati wa hafla hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...