Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Edward Marks (kushoto), akisalimiana na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) , Rished Bade (kulia) katika hafla iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake, baadhi ya wafanyabiashara na watendaji kutoka taasisi mbalimbali ili kufahamiana. Hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Katikati ni Ofisa Fedha Mkuu wa NBC, Jaffari Matundu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Edward Marks (wa pili kulia), akizungumza na baadhi ya wateja pamoja na maofisa wa benki hiyo katika hafla iliyoandaliwa na NBC kwa ajili ya wateja wake, baadhi ya wafanyabiashara na watendaji kutoka taasisi mbalimbali ili kufahamiana. Hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Edward Marks (katikati), akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Chemi Cotex, Lakshmi Narayan Rathi (kulia) katika hafla iliyoandaliwa na NBC kwa ajili ya wateja wake, baadhi ya wafanyabiashara na watendaji kutoka taasisi mbalimbali ili kufahamiana. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Ofisa Fedha Mkuu wa NBC, Jaffari Matundu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Edward Marks (kulia), akifurahi na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Sukari ya Kilombero Sugar, Ephraim Mafuru (kushoto) katika hafla iliyoandaliwa na NBC kwa ajili ya wateja wake, baadhi ya wafanyabiashara na watendaji kutoka taasisi mbalimbali ili kufahamiana. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam. Wa pili kushoto ni Kaimu Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Rukia Mtingwa na Meneja Mahusiano wa benki hiyo, William Kallaghe.
Kamishna Mkuu wa TRA, Rished Bade (katikati) akilakiwa na Ofisa Fedha Mkuu wa Benki ya NBC, Jaffari Matundu (kushoto) alipokwenda kuhudhuria hafla hiyo. Kulia ni Theobald Sabi wa NBC.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...