Na Maryam Kidiko-MaelezoZanzibar  
     
Mwanaharakati  wa  Masuala ya Wanawake wa Jimbo la Mwana kwerekwe  Bi Rihi Haji Ali amewataka Wanawake wenzake  kujitokeza kwa wingi kugombania nafasi mbali mbali za Uongozi ili kuweza kutetea haki zao .

Hayo ameyasema  huko Mwanakwerekwe wakati akizungumza na Waandishi wa habari katika suala zima la wanawake kuacha woga na kujitokeza kwa wingi kugombania  ili waweze  kujisemea wenyewe na kupata haki zao za kimsingi. 

Hata hivyo amesema wakati umefika kwa Wanawake kujisemea wenyewe na kuacha tabia ya kusemewa matatizo yao jambo ambalo linarudisha nyuma na kuchelewa kupata haki zao za msingi wanazokusudia. 

Amesema kuwa Wanawake  watapojitokeza kwa wingi  na kuwa na ushirikiano mkubwa wataweza kutetea haki zao za msingi hasa katika suala zima la udhalilishaji  unaojitokeza  hapa Nchini kwa wanawake hao.

Vile vile amesema indapo watajitokeza Wanawake kugombani nafasi hizo watatoa ushirikiano mkubwa wa kumpigia kura ili kuwapa hamasa wanaume na wao waweze kuwaunga mkono katika kugombania nafasi hizo.

“Mwanamke yoyote akijitokeza  kugombania Uongozi  tutatoa ushirikiano mkubwa na kuhakikisha anapita katika ushindani huo”Amesema mwanaharakati huyo. Amefafanuwa kuwa wanajitahidi kutoa Elimu sehemu mbali mbali na kuwaelimisha Wanawake jinsi ya kugombea na kuacha imani potofu zinazosemwa Katika Jamii. 

Hata hivyo amesema wataunda Kamati Ndogo ndogo ili kuhakikisha kila Mwanamke aliyekuwa na vigezo vya kugombania nafasi yoyote ya uongozi kuweza kupata nafasi hiyo.

Mwanaharakati huyo ameishukuru Jumuiya   ya Waandishi wa habari Wanawake  Tanzania (TAMWA) pamoja na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kwakuweza kuwatetea Wanawake na kuhakikisha wanapata haki zao za msingi.

Sambamba na hayo amevitaka Vyombo vinavyotoa  Elimu kuhusu masuala ya Wanawake na kuzidi kutoa Elimu kwa Wanawake na kuwataka Wanawake kutoa mashirikiano pamoja na kupendana ili kutimiza lengo walilokusudia.
                                                             
                                 IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...