Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
MAJIMBO mapya ya uchaguzi kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) mwishoni mwa Juni, ili kuweza majimbo hayo kupata wabunge watakaowakilisha wananchi hao.

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,Kaimu Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ,Kailima Ramadhani amesema ugawaji huo utakuwa umezingatia idadi ya watu,jiografia ya eneo husika pamoja mawasiliano na uchumi ili kuweza kuwalishwa na bunge katika maendeleo ya jimbo.

Ramadhan amesema katika Wilaya mpya zote zinaingia katika jimbo la uchaguzi kinachobaki ni kupata maombi ya majimbo mengine kutoka kwa Makatibu Tawala wa Mikoa (RAC).

Amesema kuwa baada ya maombi hayo tume ya Uchaguzi ya Taifa itapitia mipaka pamoja na kugawa kata kutokana na kata moha haiwezi ikawa katika majimbo mawili.

“Tunachotaka ni makatibu Tawala wa Mikoa kuleta maombi yao mapema na kuweza kuyapitia na katika mipaka pamoja na vigezo vilivyoanishwa na NEC”amesema Ramadhan.
 Kaimu Mkurugenzi Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kailima Ramadhan akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC), juu ya ugawaji wa majimbo mapya ya uchaguzi jijini Dar es Salaam leo.
 Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa NEC akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari hawapo pichani walipokutana leo jijini Dar es Salaam.
  Baadhi ya   wanahabari wakifuatilia katika mkutano wa NEC uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.(PICHA NA EMMANUEL MASSAKA,GLOBU YA JAMII)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...