Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
WAKALA wa Huduma  za Misitu Nchini (TFS),wamewataka wawekezaji wawekeze kwenye sekta  ya ufugaji nyuki  ili kutoa matokeo mazuri katika sekta hiyo.
 Hayo yamezungumzwa na Afisa ufugaji nyuki  mkuu  wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania Mwanahamisi Mapolu wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idara ya habari MAELEZO jijini Dar es Salaam leo.
 Mapolu amesema kuwa  wawekezaji wajikite zaidi katika usimamiaji wa viwanda  vitakavyozalisha vifaa vya kufugia nyuki,visigina asali na mavazi ya kujikinga  wakati wa kulina asali.
Pia wawekezaji wajikite zaidi katika usimamiaji wa  viwanda vitakavyo zalisha bidhaa zitokanazo na nta kama mishumaa , rangi za viatu, vilainisho pamoja na vipodozi.
Mapolu amesisitiza kuwa  sera ya ufugaji nyuki nchini inahimiza ushirikishwaji wa wananchi katika shughuri za nyuki, uhifadhi mazingira na uzallishaji wa mazao ya nyuki yanayokidhi mahitaji ya soko.
Pia sera ya  Taifa ya  ufugaji nyuki nchini inasema kuwa ili kuhakikisha kuwa kuna mfumo thabiti wa biashara ya mazao ya nyuki, udhibiti wa ubora wa mazao hayo ukaguzi na utaimarishwa. Biashara ya mazao ya nyuki itahimizwa kwa kuimarisha huduma za kuaminika za udhibiti wa ubora  na ukaguzi wa mazao hayo.
Afisa Ufugaji Nyuki  Mkuu  wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)Mwanahamisi Mapolu akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari katika ukumbi wa habari Maelezo jijini Dar es Salaam leo, kushoto ni Afisa Nyuki Masoko na Leseni, Nuru Tengeza na kulia ni Afisa Ufugaji Nyuki Mkuu,Magori Nyachari.
Afisa Nyuki Masoko na Leseni, Nuru Tengeza akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusiana na Wakala wa Huduma  za Misitu Nchini (TFS) katika ukumbi wa  Idara ya habari MAELEZO jijini Dar es Salaam leo,Afisa Ufugaji Nyuki  Mkuu  wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)Mwanahamisi Mapolu.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria katika  mkutano  wa Wakala wa Huduma  za Misitu Nchini (TFS), leo jijini Dar es Salaam.Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...