Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Bw. Nachoa Zacharia kulia akiongea na ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakati wa Maafisa hao walipokuwa katika ziara ya mafunzo stadi za maisha,ujasiriamali na elimu ya uongozi kwa vijana wa Mkoa wa Ruvuma, kushoto kwake ni Mkuu wa Chuo cha Vijana cha Sasanda kilichopo mkoani Mbeya Bw. Laurian Masele.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mh. Charles Mhagama akisisitiza jambo kwa maafisa kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakati wa ziara ya mafunzo ya stadi za maisha,ujasiriamali, mfuko wa Vijana na elimu ya uongozi kwa vijana wa Mkoa wa Ruvum, kulia Afisa Vijana kutoka Wizarani Bi. Amina Sanga na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria Bi. Ester Riwa.
Afisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, na Michezo Bi. Amina Sanga akitoa mada ya jinsi ya Vikundi vya vijana wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea vilivyokidhi vigezo vinavyoweza kunufaika na mfuko huo,mafunzo hayo yamefanyika mkoani Ruvuma.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria Bi. Ester Riwa akitoa mada juu ya Sera ya Maendeleo ya Vijana ya Mwaka 2007, Stadi za Maisha na ujasiriamali kwa Vijana wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.(Picha na Benjamin Sawe).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...