Na Victor Mariki - Ofisi ya Makamu wa Rais

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais ( Mazingira), Dk. Binilith Mahenge amesema kuwa Serikali inaendelea  kukabiliana na changamoto za uharibifu  wa mazingira kwa kuhamasisha utekelezaji  wa mipango  ya kitaifa ya kuhifadhi mazingira pamoja na miongozo yake.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa maandalizi ya  maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo hufanyika  tarehe 5 Juni kila mwaka ambapo mwaka huu maadhimisho hayo yatafanyika jiji la Milani nchini Italia kimataifa na kitaifa yatafanyika mkoa wa Tanga.

Aidha Waziri Mahenge, alibainisha baadhi ya sababu za kuichagua Tanga kuwa sehemu ya maadhimisho hayo  ni kutokana na changamoto za mazingira zinazoukabili mkoa huo ikiwemo uvuvi haramu, uharibifu vyanzo vya maji, mmomonyoko wa fukwe pamoja na  kuzama kwa visiwa vya  Maziwe kutokana na mabadiliko ya tabianchi.

Aliongeza kuwa ujumbe wa  maadhimisho ya siku hiyo mwaka huu unasema " Ndoto Bilioni Saba. Dunia Moja. Tumia Rasimali kwa Ungalifu."  ambapo alifafanua kuwa ujumbe huo unahimiza jamii katika umuhimu wa utumiaj endelevu wa rasimali kwa faida zao na kwa kizazi kijacho kwa kuzingatia ongezo la watu duniani lilofikia bilioni saba kwa sasa.

Sanjari na hayo Waziri Mahenge alitoa wito kwa kila mkoa kutekeleza shughuli za kuhamasisha uhifadhi wa mazingira kwa kudhibiti uvunaji miti, kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala ya kuni na mkaa, kupanda miti inayofaa kwenye vyanzo vya maji na kuvitaka viwanda vizingatie uzalishaji bora utakaopunguza  gesijoto na kuwa na mifumo mizuri ya majitaka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...