Mradi wa Kilimo cha Tangawizi wa kikundi cha ujasiriamlai chaushindi kilichopo katika kijiji cha Mkongotema kata ya Mkongotema tarafa ya Madaba Halmashauri ya Songea.
Na Benjamin Sawe.
Katika ulimwengu wa sasa wenye changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira na ushindani wa kila namna ujasiriamali unabaki kuwa dhana pekee inayoweza kuwakomboa vijana kiuchumi na kuwawezesha kutimiza malengo na ndoto walizonazo.
Kutokana na kukithiri kwa idadi kubwa ya vijana wanaohitimu katika ngazi mbali mbali za elimu hasa elimu ya msingi,sekondari na Chuo ile hali hawana ajira na kuishia kukaa mitaani kutokana na elimu waliyoipata iliwaandaa kuajiriwa maofisini na sio kujiajiri,ni ukweli usiopingika kwamba elimu ya ujasiriamali inahitajika kwa kiasi kikubwa ili kuleta ukombozi wa kweli wa kiuchumi.
Mafanikio ni shilingi yenye pande mbili kuajiriwa na kujiajiri ,vijana wasifikiri kuwa kuajiriwa ndio njia pekee ya kufanikiwa pia wajue kuwa kuna mafanikio ya kiuchumi nje ya ajira na haya ni kwa wale walioamua kujiajiri kwa kuanzisha miradi mbali mbali ama biashara na huo ndio ujasiriamali wenyewe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...