Vijana wakiwa katika Maandamano nchini Burundi

Watu wanne wamefariki dunia na wengine tisa kujeruhiwa katika maandamano ya kupinga hatua ya Rais Pierre Nkurunziza kuwania Urais kwa Mhula wa tatu.
Mamia ya watu wamejitokeza kwenye maandamano hayo huku baadhi wakichoma moto baadhi ya vitu katika nchi hiyo.
Siku ya jumanne Mahakama ya Katiba ilikubali kuwa Rais Nkurunziza anaweza kugombea urais ambapo ilisema ni halali yeye kuwania tena urais kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
Katika hotuba yake siku ya jumatano Rais Nkurunziza alisema kama atachaguliwa tena kuongoza nchi hiyo, mhula huu utakuwa wa mwisho kwake kuwa madarakani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 08, 2015

    Amani amani Burundi kutafuta kazi kwa wanasiasa kusisababishe mauaji.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...