Baadhi
ya wakazi wa Kata ya Nyakanazi Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera
wakiwa kwenye mkutano wa kampeni
ya kutoa elimu kuhusiana na Fistula inayowakabili wanawake hapa nchini,Kampeni
hiyo inayoendeshwa na Hospitali ya CCBRT kwa kushirikiana na Vodacom Tanzania kwa
kupitia taasisi yake ya Vodacom Foundation imezinduliwa mwishoni mwa wiki na itafanyika
katika mikoa mitatu kuwasisitiza wakina mama kujitokeza ili wakatibiwe maradhi
hayo kwani yanatibika. Inakadiriwa kwa mwaka wastani ya wanawake 2,500-3,000 hupatwa
na maradhi hayo wanapojifungua
Wakazi
wa kata ya Nyakazanazi Wilaya ya
Biharamulo mkoani Kagera wakifuatilia
elimu iliyokuwa ikitolewa na wataalam kutoka hospitali ya CCBRT na
balozi wa Fistula hapa nchini Mrisho Mpoto(hawapo pichani) kuhusiana na maradhi
ya Fistula yanayowapata wanawake hapa nchini wanapojifungua. Elimu hiyo
ilitolewa wakati wa Kampeni inayoendeshwa na Hospitali ya CCBRT kwa
kushirikiana na Vodacom Tanzania kupitia taasisi yake ya Vodacom Foundation iliyozinduliwa mwishoni mwa wiki na
itafanyika katika mikoa mitatu kuwasisitiza wakina mama kujitokeza ili
wakatibiwe maradhi hayo kwani yanatibika. Inakadiriwa kwa mwaka wastani ya
wanawake 2,500-3,000 hupatwa na maradhi hayo
wanapojifungua.
Doricas
George( 26) Mkazi wa Kata ya Nyakanazi Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera
(kushoto)akijibu maswali mbalimbali kuhusiana na maradhi ya Fistula
aliyokuwa akiulizwa na Balozi wa maradhi hayo Mrisho Mpoto(kulia)alipokuwa akitoa
elimu kuhusiana na maradhi hayo inayoendelea kutolewa katika mikoa mitatu
nchini ikiwa ni mwendelezo wa kampeni ya kusisitiza wakina mama kujitokeza ili
wakapatiwe matibabu katika hospitali ya CCBRT kwa kushirikiana na taasisi ya
Vodacom Foundation kutokomeza janga hilo.Katikati ni Meneja Biashara Idara ya Uhusiano wa Vodacom
Tanzania,Grace Lyon.
Wakinamama wakazi wa kata ya Nyakanazi Wilaya ya Biharamulo mkoa wa
Kagera wakimsikiliza kwa makini Meneja Biashara Idara ya Uhusiano wa Vodacom
Tanzania,Grace Lyon alipokuwa akiwafafanulia jambo kuhusiana na elimu ya maradhi
ya Fistula wakati wa Kampeni ya kutokomeza maradhi hayo hayo inayoendelea
kutolewa katika mikoa mitatu nchini ikiwa ni mwendelezo wa kampeni ya
kusisitiza wakina mama kujitokeza ili wakapatiwe matibabu katika hospitali ya
CCBRT kwa kushirikiana na taasisi ya Vodacom Foundation kutokomeza janga hilo. Inakadiriwa
kwa mwaka wastani ya wanawake 2,500-3,000 hupatwa na maradhi hayo wanapojifungua.
Meneja Biashara Idara ya Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Grace
Lyon akitoa elimu kwa wakazi wa kata ya Nyakanazi Wilaya ya Biharamulo Mkoa wa
Kagera,kuhusiana na maradhi ya Fistula wakati wa mwendelezo wa Kampeni ya
kutokomeza maradhi hayo inayoendelea kutolewa katika mikoa mitatu nchini ikiwa
ni mwendelezo wa kampeni ya kusisitiza wakina mama kujitokeza ili wakapatiwe
matibabu katika hospitali ya CCBRT kwa kushirikiana na taasisi ya Vodacom
Foundation kutokomeza janga hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...