3.jpg pichaBodi ya taasisi ya UTT-PID na Menejimenti yake wakia katika picha ya pamoja na uongozi wa kampuni ya Chengdu Engineering Corporation wakati wa picha ya pamoja. Waliosimama mbele (wa pili kutoka kulia) ni mjumbe wa bodi Bi. Janeth Mmari, akifuatiwa na Mkurugenzi Mkuu wa UTT-PID, Dr. Gration Kamugisha, akifuatiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya UTT-PID, Mrs Elpina Mlaki. Wengine ni wajumbe wa bodi hiyo ya UTT-PID pamoja na wenyeji wao wa nchini humo 

Na Mwandishi Maalum
Bodi ya Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu iliyo chini ya Wizara ya Fedha (UTT-PID), pamoja na Menejimenti yake iliyozuru nchini China katika ziara maalum ya siku tano kwa ajili ya Mafunzo na kubadilishana uzoefu imefana na tayari bodi hiyo imerejea nchini.

Katika ziara hiyo, Bodi ya UTT-PID, ikiongozwa na mwenyekiti wake Mrs. Elipina Mlaki pamoja na Menejimenti nzima walieleza kuwa imeweza kuwa ya mafanikio makubwa huku wakiahidi kuyafanyia kazi yae yote waliojifunza nchini China.

Katika ziara hiyo, bodi na menejimenti ya UTT-PID walipata wasaha wa kutembelea maeneo mbalimbali ya miji ya nchi hiyo ikiwemo makampuni makubwa na kujifunza na kujenga na kudumisha ushirikiano wa utendaji wa kazi.
2.jpg
Mwenyekiti wa Bodi ya UTT-PID, Mrs. Elpina Mlaki (wa pili kulia) akilezea jambo katika moja ya mkutano wao waliofanya katika ziara hiyo nchini China. Anayemfuatia ni Mkurugenzi Mkuu wa UTT-PID, Dr. Gration Kamugisha pamoja na wajumbe wa bodi na Menejimenti ya UTT-PID, Wengine kushoto ni watendaji kutoka kampuni ya Chengdu Engineering Corperation ya nchini humo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...